• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZAZI MSIWANYANYAPAE WATOTO WENYE DOWN SYNDROME - RC MTAND

Posted on: March 21st, 2025

WAZAZI MSIWANYANYAPAE WATOTO WENYE DOWN SYNDROME  - RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa jamii kuwajali watoto wenye tatizo la Down Syndrome na kuhakikisha wanawapatia huduma za kijamii kama elimu na afya na kuacha tabia ya kuwatenga na kuwanyanyapaa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo tarehe 21 Machi, 2025 wakati akihutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Down Syndrome Kitaifa kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Maadhimisho yaliyofanyika katika viwanja vya Furahisha.

"Watu wenye ulemavu wana uwezo wa kufanya mambo makubwa sana, tusiwafiche watoto wenye tatizo hili wala ulemavu wa aina yoyote, na tuwakumbushe kuwa watakaowalea vizuri wenye tatizo hili basi mbele ya Mwenyezi Mungu wana daraja na fungu lao la thawabu." Mhe. Mtanda amefafanua.

Aidha, ametoa wito kwa watoa huduma za kijamii mathalani sekta ya afya kuhakikisha wanafuatilia utekelezaji wa matamko ya Serikali na namna ya kutekeleza katika kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa kundi hilo kwa mujibu wa sera ya afya inavyotambua kisheria.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewataka wazazi wanapokuwa wajawazito wafanye hima kufika kwenye vituo vya huduma kwa uchunguzi na kufuata ushauri wa wataalamu na amebainisha kuwa Usonji inasababishwa na Chromosome kuzidi hadi 47 kutoka 46 za kawaida kwa binadamu na kusababisha kuwa na zaidi ya mfumo wa jinsi ya ukuaji wa ubongo na mwili na kwamba wenye hali hiyo wakipata msaada wanaweza kukua kiafya na kuwa na furaha na kuleta tija katika jamii wanayoishi.

Naye, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Down Syndrome nchini Bi. Mony Teri Pettit ametoa wito kwa Serikali kuhakikisha kunakuwepo na mifumo bora ya kupata huduma za kijamii inaboreshwa hususan elimu na afya kwa kupatiwa huduma hizo na bila malipo na kujumuishwa kwenye stadi mbalimbali.

Bi. Anna Barnabas Mzazi wa mtoto mwenye Down Syndrome amewataka wazazi kuwalea watoto wenye tatizo hilo kwa upendo na ameiomba Serikali kufanya vipimo mara tu mtoto anapozaliwa ili kuwabaini na siyo kubahatisha katika matibabu kama ambavyo mwanaye alikosewa na kumsababishia kushindwa kuzungumza hadi sasa.

Siku ya Kimataifa ya Down Syndromes ambayo kitaifa imefanyika Mwanza imepata heshima ya kuadhimisha imechagizwa na kaulimbiu isemayo ; Mifumo ya Huduma za Kutuwezesha Iboreshwe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.