• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI MKUU ATOA WITO KWA VIJANA KUACHANA NA MATUMIZI NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA

Posted on: June 30th, 2024

WAZIRI MKUU ATOA WITO KWA VIJANA KUACHANA NA MATUMIZI NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb.) amewataka Vijana wa Kitanzania kuachana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya na badala yake waungane katika kufanya shughuli halali za kiuchumi ili wajiletee maendeleo katika ngazi ya familia, jamii na hata Taifa.

Waziri Mkuu ametoa wito huo leo Juni 30 2024, alipokuwa akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Kitaifa ya kupiga vita dawa za kulevya duniani ambapo Kitaifa yamefanyika Jijini Mwanza kwenye uwanja wa  Nyamagana.

"Nitoe wito kwa vijana tuachane na dawa za kulevya na tujikite katika kujenga familia zetu kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kujiletea maendeleo",Waziri Mkuu

Mhe. Majaliwa amesema ili kuondokana na janga la matumizi na biashara ya dawa za kulevya ni lazima kudhibiti kwanza kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu athari zitokanazo na matumizi ya dawa hizo.

"Ni lazima tuimarishe mikakati yetu ya kukabiliana na mapambano dhidi ya dawa za kulevya na Serikali imejikita katika kutoa elimu ili jamii ifahamu, na tutakwenda kuanzia klabu za mapambano na tutaanzia katika shule za Msingi, Sekondari mpka Vyuo Vikuu kama walivyofanya TAKUKURU",Mhe.Majaliwa

Aidha Waziri Mkuu pia amesema kwa sasa Serikali pia imeongeza upana kidogo na sasa wanagusa nyanja nyingi kwanza wanachi watambue madhara ya matumizi ya dawa za kulevya lakini pia wanawawezesha waliotoka huko (Waraibu) ili waweze kujumuika na wenzao wafanye kazi na waweze kujisimamia.

Kadhalika Mhe. Majaliwa amewataka wananchi waliojitokeza uwanjani hapo kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelimisha wale wote ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika maadhimisho hayo kuhusu athari na madhara ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya kwa ustawi wa jamii na Taifa letu kiujumla.

"Dawa hizi, bangi hizi si nzuri, mkawaambie wasikubali kupewa  popote unaweza ukapewa cha arusha na utalala hapo hapo ukapotea, hata skanka hii inatisha kwanza jina lenyewe tu linatisha msitumie mtapotea",amesisitiza Mhe.Majaliwa

Pia Waziri Mkuu amesema ni mpango wa Serikali sasa katika kuhakikisha waraibu wote wa matumizi ya dawa za kulevya wanapewa huduma ya matibabu kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali ambapo kwa sasa Serikali inaboresha kwanza huduma za afya kisha waanze kuratibu mpango huo.

"Kwa sasa huduma za matibabu kwa waraibu wa dawa za kulevya zinapatikana katika Vituo 16 nchini na kuwafanya wenye uraibu kupatiwa tiba na elimu".

Kama katika jamii kuna kijana ambaye ni mraibu msisite, mumpeleke katika vituo hivyo lakini pia hata kwa hapa Mwanza Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure inatoa huduma ya matibabu kwa waraibu wa dawa za kulevya. Amesema Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amewasihi Watanzania kuhakikisha wanaunganisha nguvu kwa pamoja na kwamba aina yoyote ya dawa za kulevya Tanzania sio mahali sahihi kwake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.