• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

Posted on: January 23rd, 2026

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 23 Januari, 2026 amezindua rasmi meli mpya ya kisasa ya Mv. New Mwanza iliyojengwa na Mkandarasi Gas Entec Ship- Building kutoka Korea kwa gharama ya Tshs. Bilioni 120.56.

Akizungumza na wananchi katika eneo la Bandari ya Mwanza Kusini Mhe. Waziri Mkuu amesema kuwa ujenzi wa Meli hiyo ya kisasa ni ishara ya juhudi za serikali kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuhakikisha wanamaliza kiu ya kuwa na usafiri imara katika ziwa Victoria.

Aidha, ameiagiza Wizara ya Uchukuzi kuendeleza ujuzi uliotumika kujenga meli hiyo, TASHICO washirikiane na wadau wengine kulinda mradi huo kwa kuweka bima na kufuata ushauri wa kitaalamu na kuimarisha na kukuza diplomasia ya mahusiano na amani.

Halikadhalika, ameziagiza wizara zinazosimamia miradi ya maendeleo mathalani miundombinu kufanya tathmini kubaini miradi ambayo wakandarasi hawajalipwa fedha ili walipwe na ikamilike kama mradi huo wa meli na kuleta tija kwa jamii.

“Naomba niwaagize Mawaziri wa kisekta, fanyeni tathmini kwenye miradi yote ambayo mikataba imeshasainiwa lakini wakandarasi hawajapata fedha za awali na wizara ya fedha pitieni mafungu yote isipokuwa ya vyombo vya usalama na Afya mkate mpeleke fedha kwenye miradi hii ili ikamilike.” Waziri Mkuu.

“Wakati serikali ya awamu ya sita inaingia madarakani ilikuta meli hii imejengwa kwa 40% zikiwa zimelipwa Tshs. Bilioni 40.64 tu, tunamshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kulipa Tshs. Bilioni 79.98 na kuwezesha mradi huu kukamilika.” Amesema Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa.

“Meli hii itaboresha utoaji na upatikanaji wa huduma kwa wananchi, mathalani kupunguza adha za usafiri kwa wananchi walizokuwa wakizipata au kupeleka bidhaa zao nje ya Mwanza kama vile Mkoa wa Kagera na Nchi Jirani za Kenya na Uganda.” Amesema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.