• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Majaliwa aagiza Wananchi wa eneo la Fela kupimiwa viwanja ili kunufaika na mradi wa SGR

Posted on: October 16th, 2022


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Misungwi  mkoani Mwanza  Benson Mihayo

 kupima viwanja eneo la Fela ili wananchi  waweze kunufaika na uwepo wa bandari kavu inayotarajiwa kujengwa katika  eneo hilo.

Mhe. Majaliwa amesema hayo leo Oktoba 16, 2022 akiwa eneo la Fela  Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza   baada ya kukagua maendeleo ya  ujenzi wa Reli ya kisasa(SGR) kipande kinachoanzia Isaka hadi Mwanza chenye urefu wa kilomita 341 kinachojengwa kwa gharama ya Shilingi Trilioni 3.06 .

Amesema viwanja vilivyopo eneo hilo vikipimwa vitawanufaisha wananchi kwani wenye uwezo wa kifedha wataweza kujengwa hoteli na nyumba  za kulala wageni hivyo kujiongezea kipato wao na Taifa kwa jumla.

Aidha, Mhe. Majaliwa amewataka watanzania waliopata nafasi ya kuajiriwa kwenye mradi huo kufanya kazi kwa weledi na bidii huku wakizingatia mafunzo wanayoyapata  maana Serikali inawategemea kwa ajili ya kuteleleza miradi mingine.

"Mkifanya kazi kwa weledi nawahakikishia mtaisaidia sana Serikali maana ujuzi mnaoupata kutoka kwa wakandarasi wageni wakiondoka tukianzisha miradi mingine Serikali itawatumia nyie hivyo tutapunguza gharama za kuleta wataalamu wa kigeni kutoka nje ya nchi,"ameongeza.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema mradi huo ambao ujenzi wake umefikia asilimia 14.12 ni mhimili mkubwa na thabiti katika ukuaji wa uchumi wa taifa maana ukikamilika  utaleta mapinduzi katika sekta za viwanda, kilimo, ujenzi, ufugaji, usafirishaji, madini pamoja na utalii.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Amina Lumuli amebainisha kwamba mradi huo umekuwa na mafanikio mengi kwa watanzania kwani hadi Septemba 30, 2022 ulikuwa na jumla ya wafanyakazi 5,897 kati ya hao 5,384 sawa  na asilimia 91.3 ni watanzania na 513 sawa na asilimia 8.7 ni raia wa kigeni.

Ameongeza kuwa TRC imeendelea kutoa mafunzo ya  vitendo kwa wataalamu wake mbalimbali, mafunzo hayo yamekuwa na tija sana kwani zaidi ya wataalamu 40 wanashiriki moja kwa moja kwenye ujenzi wa mradi wa  SGR.

" Mradi huu ukikamilika utakuwa na faida mbalimbali ikiwemo kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa abiria na mizigo kwa kupunguza muda wa safari mathalani kutoka jijini Dar es Salaam  hadi Mwanza kutoka masaa 18 hadi 20 ya awali hadi nane, vilevile  utachochea uanzishwaji  wa miji midogo katika sehemu zinazojengwa stesheni ambazo zitakuwa kivutio kwa wananchi.

" Pia utapunguza  gharama za usafirishaji mizigo kati ya asilimia 30 hadi 40  na kuifanya bandari ya Dar es Salaam kuhimili ushindani, utachochea uanzishwaji wa viwanda maeneo mengine ya nchi kutokana na uwepo wa uhakika wa usafirishaji wa malighafi na bidhaa,"ameeleza.

Mhe. Majaliwa yuko Mkoani Mwanza  tangu Oktoba 15 ,2022, kwa ziara ya siku nne ya kikazi lengo likiwa ni kukagua maendeleo ya miradi ya  kimkakati inayotekelezwa na Serikali pamoja na kukutana na wananchi ili kuwaeleza kuhusu  miradi  mbalimbali ambayo serikali ya awamu ya sita inaitekeleza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.