• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Majaliwa asisitiza nidhamu ya matumizi ya fedha za miradi

Posted on: October 17th, 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) ametaka kuwepo na nidhamu nzuri ya matumizi ya fedha za Miradi ya Maendeleo akitoa mfano wa kuigwa Wilaya ya Ukerewe Kisiwa cha Irugwa.

Akizungumza leo Kisiwani Irugwa wakati wa ukaguzi wa vyumba vya madarasa 6 shule ya Sekondari Irugwa vilivyogharimu Tshs milioni 120 na kutumika Tshs milioni 119, Mhe. Majaliwa amesema kwa jiographia ya Kisiwa hicho na nidhamu ya matumizi ya fedha hizo wahusika wote wanastahili pongezi.

"Leo nawapa zawadi ya Tshs Milioni moja mkagawane kwa nidhamu mliyoonesha maana natambua changamoto ya kuleta Vifaa hapa vya ujenzi lakini bado mmetumia fedha vizuri na chenji kubaki, Viongozi wengine nataka wapate ujumbe huu." Amesisitiza  Waziri Mkuu.

Mhe. Majaliwa amebainisha kuwa bado kuna changamoto sana ya matumizi ya fedha za Serikali zinazolengwa kuwaletea Maendeleo wananchi na kusisitiza hatakuwa na huruma Kwa Viongozi wenye tabia hizo.

Aidha, Waziri Mkuu ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kisiwani Irugwa kilichogharimu Tshs milioni 500 na kuahidi kuletwa kiasi cha Tshs milioni 270 kwa ajili ya kukiboresha Kituo hicho kiwe na matibabu yote ya msingi likiwemo jengo la Mama na Mtoto.

Akijibu hoja ya Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe Denis Mwila kuhusiana na ubabaishaji wa Mkandarasi wa barabara za ndani mjini Nansio kampuni ya Inter Country inayomilikiwa na Mazoa Nyakilagani, Mhe. Majaliwa ameagiza Mkandarasi huyo kufika Ofisini kwake Dodoma wiki hii ili kujibu tuhuma za kuzembea kukamilisha Mradi huo.

Kuhusu kero ya usafiri wa Mitumbwi Kisiwani humo Mhe. Majaliwa amewaahidi Wakazi hao kulibeba suala hilo na kwenda kulifanyia kazi ili wapate kivuko cha uhakika.

Awali akimkaribisha Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema Mkoa huo umeendelea kunufaika na Miradi mbalimbali ya Maendeleo kuanzia Sekta ya Afya, Elimu na Miundombinu.

"Mhe. Waziri Mkuu Kisiwa cha Irugwa kipo mbali sana kutoka mjini Nansio na wakazi wa huku huduma za haraka kwao wanazipata Mkoani Mara ambako ni karibu hivyo kuwaletea huduma zote za msingi hapa kutawapunguzia usumbufu," amesema Mkuu wa Mkoa.

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa anaendelea na ziara yake mjini Mwanza kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Stendi ya m

Mabasi ya Nyegezi na ujenzi wa Meli mpya Mv Mwanza Hapa Kazi tu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.