• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Mhe.Majaliwa azitaka Halmashauri zote nchini kutunga Sheria rafiki kwa Wachimbaji wadogo wa Madini

Posted on: May 9th, 2023

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb)  amezitaka Halmashauri  zote kutunga sheria ambazo zitakua ni rafiki kwa wachimbaji  wadogo wa madini kwa kuhakikisha wanashirikiana  na wadau katika mapendekezo ya utungaji wa sheria ndogo ndogo.

Mhe. Majiliwa ameyasema hayo leo Mei 9, 2023   alipowasili Jijini Mwanza kwa ajili ya ufunguzi wa  Kongamano la Wachimbaji Wadogo wa Madini na Mkutano Mkuu wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa Madini (FEMATA)  ambalo limefanyika  katika ukumbi wa Rock City Mall.

" Nawaelekeza Mameya wa Halmashauri nyie ndio mnaotunga sheria ndogo muwe mnahakikisha mnawashirikisha  wadau katika mapendekezo ya utungaji wa sheria ndogo ili msiwe mnatunga sheria ambazo zitakuwa zinawaumiza watumiaji wa sheria hizo," Amesema Mhe. Majaliwa

" Sekta ya madini imekuwa ikitoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi na kongamano hili lina fursa kubwa kwetu katika kuzitoa changamoto zetu ili kuongeza tija katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia sekta ya madini," Ameongeza Mtendaji Mkuu huyo wa Serikali.

Aidha Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Kiruswa akizungumza kwa niaba ya  Waziri wa Madini  Mhe. Dkt Dotto Biteko  amemuahidi Mhe. Majaliwa kuwa   Wizara yake  itaendelea kupokea  na kusimamia mikakati inayotolewa na serikali.

" Mhe. Waziri Mkuu nakuahidi kuwa Wizara itaendelea kupokea na kusimamia  mikakati  inayotolewa na serikali ili kuhakikisha inaongeza kasi katika kuchangia maendeleo nchini," Amesema Mhe. Dkt. Kiruswa

Pia  Mhe. Adam Malima Mkuu wa Mkoa wa Mwaza ameiomba Wizara ya Madini na Shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa Madini (FEMATA) kuja kufanya kongamano lijalo la Mwaka 2024 mkoani humo

" Mhe. Mgeni rasmi kama kauli mbiu yetu inavyosema kwamba amani iliyopo  Tanzania itumike kuwa fursa ya kiuchumi na Tanzania kwa kitovu cha biashara ya madini Afrika tunaiomba serikali iunde chombo maalum ambacho kitashughulika na suala la amani ili kukuza uchumi," Amesema  Ndg. John Binna,Rais wa FEMATA

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa  amefungua kongamano hilo la  Madini na Mkutano Mkuu wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa Madini (FEMATA) ikiwa ni maagizo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.