• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WEKEZENI KATIKA MICHEZO NI AJIRA YA UHAKIKA KWA WANAMICHEZO-RC MAKALLA

Posted on: July 28th, 2023

WEKEZENI KATIKA MICHEZO NI AJIRA YA UHAKIKA KWA WANAMICHEZO-RC MAKALLA


*Awashauri wenye shule kuvibaini vipaji na kuweka mikakati ya kuviendeleza


*Asema wanamichezo sasa ndiyo wanaotamba Duniani kwa kupata vipato vikubwa


Wamiliki wa shule na wadau wa michezo kwa ujumla Mkoani Mwanza wameshauriwa kufanya uwekezaji wa kweli katika sekta ya michezo kwa kuvibaini vipaji na kuweka mikakati ya kuviendeleza.

Akizungumza Alhamisi hii kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana mara baada ya mchezo wa fainali soka la wanawake  ligi ya mabingwa mkoa ngazi ya Taifa kati ya Fountain Gate na Mwanga FC,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA.Amos Makalla amesema mafanikio katika michezo ni matokeo ya uwekezaji mzuri kwa kuvibaini vipaji vya wachezaji tangu hatua za awali.

Makalla ambaye amesakata kabumbu miaka ya nyuma amebainisha Ulimwemguni hivi sasa wanaotamba kwa vipato vikubwa ni wanamichezo mbalimbali ambao ni matunda ya kuandaliwa tangu wakiwa na umri mdogo.

"Tumeshuhudia mchezo mzuri wa fainali soka la wanawake umri wa wachezaji hawa ndiyo sahihi kuhakikisha wanawekewa mikakati kamambe ya kuendelezwa,mwanangu kasoma shule hii ya Fountain Gate sasa hivi yupo kwenye majaribio huko Hispania," amefafanua CPA Makalla

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mpambano huo wa fainali, amewapongeza mabingwa wa michuano hiyo timu ya Fountain Gate kutoka Dodoma kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mwanga ya Kigoma,matokeo ambayo yamewapa tiketi ya kucheza ligi daraja la kwanza msimu ujao.

Michuano hiyo ya Ligi ya mabingwa mkoa kwa upande wa wanawake ngazi ya Taifa,imeshirikisha jumla ya Mikoa 19 huku michezo hiyo  ikirindima kwenye viwanja vya Nyamagana na CCM Kirumba.

Miongoni mwa mashuhuda wa mchezo huo wa fainali ni pamoja na Rais wa Shirikisho la soka nchini,TFF Wallace Karia,Mwenyeki wa kamati ya soka la Wanawake nchini,Hawa Mniga, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mwanza,MZFA Vedasto Lufano na Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mhe.Stanslaus Mabula.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.