• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wiki ya Kitaifa ya magonjwa yasiyoambukiza yazinduliwa rasmi leo Mkoani Mwanza

Posted on: November 5th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewakumbusha wakazi wa Mkoa huo kuitumia vizuri wiki ya Kitaifa ya magonjwa yasiyoambukiza ili kujitambua mapema afya zao.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mh. Hassan Masala akizindua rasmi leo wiki hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa kwenye uwanja wa CCM Kirumba,amesema kasi ya magonjwa yasiyoambukiza imekuwa kubwa kutokana na watu wengi kutozingatia kanuni za afya likiwemo suala la kujichunguza mara kwa mara.

"Nitumie nafasi hii kuwakumbusha ndugu zangu ule usemi wa kinga ni bora kuliko tiba,haya magonjwa yamekuwa ni mzigo wa gharama na kusababisha nguvu kazi ya Taifa kupotea kutokana na vifo au kazi kuzorota,tuna kila sababu ya kuelimika kuanzia aina ya ulaji wa vyakula usiofaa na tufanye mazoezi" amesema Mhe.Masala

Ameendelea kusema wiki   hiyo itakuwa ni msaada mzuri kwa Wananchi watakaofika uwanjani hapo na kukutana na Wataalam wa Afya ambao watawafanyia vipimo na kupewa elimu.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa magonjwa yasiyoambukiza,ajali na afya ya akili kutoka Wizara ya afya Dkt.James Kiologwe amebainisha Wizara yake inaendelea kuwa mstari wa mbele kuelimisha umma kwa njia mbalimbali ikiwemo kama hii inayofanyika Mkoani Mwanza lengo likiwa watu watambue umuhimu wa kinga mapema.

"Watu wengi bado wanaishi wakiwa na maradhi kama shinikizo la damu,kisukari na saratani bila kujitambua mapema na wanapoanza kuumwa ndipo wanagundulika na matatizo hayo hali ambayo inawaletea taharuki na hofu" amesisitiza Dkt.Kiologwe

Uzinduzi wa wiki ya Kitaifa ya magonjwa yasiyoambukiza ambayo kilele chake itakuwa Novemba 12 mwaka huu, imeanza kwa Wananchi wa Mwanza kushiriki mbio pamoja na michezo mbalimbali ikiwemo soka,mpira wa pete na kikapu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.