• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wizara ya Mifugo na Uvuvi yavitaka vyama vya Ushirika kuwa chachu ya kukuza Uchumi

Posted on: January 6th, 2023


Wizara ya Mifugo na Uvuvi imevikumbusha vyama vya Ushirika kufanya kazi kwa weledi ili viwe chachu ya kuinua uchumi kwenye Sekta hiyo ambayo Serikali inazidi kuboresha mazingira yao.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega amesema hayo leo Jijini Mwanza kwenye Maabara ya Samaki wakati wa hafla fupi ya utiliaji saini baina ya Chama cha Ushirika cha Uvuvi cha Bukasiga na Ushirika wa Wataalamu wajasiriamali kutoka Chuo cha kilimo Sokoine SUGEKO ,amebainisha kuwa Serikali imeongeza zaidi ya Shs Bilioni 100 kwenye Sekta ya Uvuvi lengo likiwa kuongeza nguvu ya kuwainua wavuvi ili wafanye shughuli hiyo kisasa zaidi.

"Serikali ya awamu ya Sita katika bajeti yake ya mwaka 2022-23 ilitenga Shs bilioni 60 kwa ajili ya Uvuvi na bilioni 40 zilienda kwa wafugaji huku bilioni 20 zikilenga ufugaji wa kisasa wa samaki" amefafanua Naibu Waziri.

Aidha mwaka huu amesema wavuvi watakopeshwa boti za kisasa za Uvuvi ili lengo litimie la wavuvi kujipatia kipato zaidi.

Ameongeza kuwa Serikali imeweka benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB ili sasa watu wa Sekta hiyo kujiaminisha na shughuli zao kutokana na kuwa na uhakika wa kukopeshwa fedha tofauti na miaka ya nyuma Benki zilikuwa zikihofia kupoteza fedha zao.

"Kutokana na kasi ya kumletea maendeleo mwananchi inayo onesha Serikali sisi kama Mkoa tumeendelea kuhimiza na kutoa elimu kwa vikundi maalum kuchangamkia fursa ya Uchumi wa bluu kwa kufuga samaki wa Vizimba,mradi ambao umeonesha kuwa na tija" Emil Kasagara kaimu Katibu Tawala Uchumi na Uzalishaji

Mbunge wa Ukerewe Mh.Joseph Mkundi ameiomba Serikali kuipa kipaumbele Wilaya ya Ukerewe katika mkakati wa kuwainua wavuvi kiuchumi nchini kutokana na Wilaya hiyo  watu wake kujishughulisha na Uvuvi.

Benki ya Maendeleo ya Kilimo ilikikopesha Chama cha Ushirika cha Bukasiga kutoka Ukerewe Shs Milioni 260 mwaka 2020 kwa ajili ya mradi wa ukaushaji dagaa,hata hivyo baada ya kutokea hali ya kusuasua wa mradi huo, Ushirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo cha Kilimo Sokoine wameingia mkataba wa kuendesha mradi huo kwa kipindi cha mpito na kuchukua deni la mradi huo Shs Milioni 106,000,000.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.