• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Zaidi ya lita 92 elfu za Kemikali ya Ethyl Alcohol zakabidhiwa Mwanza

Posted on: April 20th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amepokea Kemikali bashilifu lita 92.226 aina ya Ethyl Alcohol kutoka kwa Mhakiki mali Mkoa wa mwanza Bw.Colman Shayo ili zitumike katika kutengeneza vitakasa mikono kwa ajili ya kujikinga na maambukizi yatokanayo na virusi vya corona baada ya taratibu na kesi kuamriwa na kukabidhiwa kwa serikali.


Akielezea kuhusiana na Kemikali hizo Kaimu Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya kudhibiti na  kupambana na madawa ya kulevya Bw. James Kaji alisema Kemikali hizo zilikamatwa baada ya kuingizwa nchini bila kufuata utaratinu kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kupelekwa Mahakamani na kesi kuamuliwa zilitaifishwa na Serikali.

"Tumeamua tuukabidhi Mkoa, hii ni kutokana na juhudi za Mhe.John Mongella Mkuu wetu wa Mkoa katika kupambama na janga la corona kwa jitihada alizozifanya kuonana na ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Kamati inayoshughulika na kudhibiti maambukizi ili zitumike kutengeneza vitakasa mikono,"alisema Kaji.


Akiongea kwa niaba ya Mkemia  Mkuu wa Serikali Bw. Bonventura Masamba amesema wamepokea mapipa mia tatu sitini na saba (367) yenye ujazo wa lita mia mbili hamsini (250) kila moja na kufanya jumla ya lita iahirini na moja elfu na mia tisa sabini na sita(21,976)yenye kemikali aina ya Ethin alcohol yaliyokamatwa disemba 2017 katika keai za jinai 195 na 197 za 2018.

"Mamlaka ya  Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ni taasisi ambayo pamoja na majukumu mengine iliyopangiwa na Serikali ni kusimamia uingizwaji,usafirishwaji na kudhibiti namna bora ya matumizi ya kemikali,"alisema Masamba.

Akikabidhi mali hizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella  Bw.Colman Shayo ambaye ni Mhakiki Mali wa Mkoa wa Mwanza amesema atashirikiana na Mkoa ili kuhakikisha kuwa mali hizo zinatumika kwa lengo lililokusudiwa na kuhakikisha wanatekeleza wajibu huo kwa uadilifu na utaratibu unaokubalika na Serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amesema katika vita dhidi ya kupambana na madawa ya kulevya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama waliaimamia kikamilifu na ndiyo imepelekea kupatikana kwa kemikali hizo bashilifu.

"Tumepokea maelekezo kutoka ofisi ya Waziri Mkuu na sisi hapa tunachofanya baada ya wenzetu kutoka Dodoma na Dar es Saalam ni kupokea kubwa ni kwamba tunaahidi kuaimamia kwa uadilifu na weredi kazi hiyo ya kutengeneza vitakasa mikono na kuhakikisha kwamba kemikali hizi hazirudi tena sokoni maana yake tayari ziliishakamatwa,"alisema Mhe.Mongella.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.