• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA WALENGWA ELFU HAMSINI WANUFAIKA NA RUZUKU YA BILIONI 82 MWANZA

Posted on: August 13th, 2025

Serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 82 kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika mpango wa kunusuru kaya maskini awamu tatu ndani ya Halmashauri nane za Mkoa wa Mwanza ambapo wanufaika zaidi ya elfu 51 wamenufaika na fedha hizo.


Akizungumza katika kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa mpango, Mkuu wa Wilaya ya Nyamgana Mhe. Amina Makilagi alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiendeleza TASAF kwa mafanikio makubwa.

Mhe. Makilagi amesema TASAF imekuwa na mafanikio makubwa katika awamu ya sita kwani idadi ya miradi ya maendeleo na wanufaika imeongezeka ukilinganisha na kipindi cha hapo nyuma.


Kupitia taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa TASAF awamu ya tatu kipindi cha pili, iliyosomwa na Mratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza Bi. Monica Mahundi amesema Mwanza ni miongoni mwa Mikoa inayotekeleza miradi ya kupunguza umaskini awamu ya nne (TPRP IV) ambapo jumla ya gharama za miradi hiyo ni shilingi 19,695,345,100.12 inatekelezwa.

“Hadi sasa, jumla ya miradi 242 inatekelezwa miradi 73 ni ya afya na 169 ni ya elimu. Miradi 175 imekamilika na miradi 67 inaendelea na utekelezaji”. Bi. Mahundi.


Kadhalika, Bi. Mahundi amesema Mkoa wa Mwanza unatekeleza Programu ya kuweka akiba na kukuza uchumi kupitia Mpango wa kunusuru kaya Maskini. Hadi sasa, Mkoa umeunda vikundi vipatavyo 3,729, kati ya hivyo vikundi 3,729 vimesajiliwa kwenye Mfumo.


Kuhusu mafanikio Bi. Mahundi amesema Walengwa 42,804 wameanzisha shughuli za kujiongezea kipato ikiwa ni pamoja na biashara ndogo ndogo, kilimo na ufugaji. Walengwa 15,608 wameweza kujenga nyumba na kuboresha makazi.


Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ni mojawapo ya mradi katika Programu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Awamu ya Tatu (TASAF III) ambao ulizinduliwa Mkoani Mwanza Oktoba 2014 na utekelezaji wake ulianza Julai 2015.


Mpango huo una lengo la kuziwezesha Kaya maskini kuongeza kipato, fursa na kuongeza ufanisi katika matumizi ya chakula, afya na elimu. Kimkoa Mpango huu unatekelezwa katika Wilaya zote 7 kwa wanufaika wanufaika 51,944.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA MTAKUWWA MWANZA YATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WA KULINDA JAMII DHIDI YA UKATILI

    August 13, 2025
  • ZAIDI YA WALENGWA ELFU HAMSINI WANUFAIKA NA RUZUKU YA BILIONI 82 MWANZA

    August 13, 2025
  • WARATIBU WA TASAF WAAGIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA UKAMILIFU NA UTIMILIFU

    August 12, 2025
  • RC MTANDA AKITETA JAMBO NA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

    August 11, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.