• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mikakati ya Maendeleo Yajadiliwa Buchosa

Posted on: September 22nd, 2019


Katika kutekeleza mikakati ya kimaendeleo inayofanywa na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,  Halmashauri ya wilaya ya Buchosa iliyopo  mkoani Mwanza ni mojawapo ya halmashauri iliyojipanga katika kutekeleza  mikakati hiyo.

Hayo yameelezwa  hii leo katika kikao cha 4 cha baraza la madiwani kilichofanyika Wilayani humo kilichoongozwa na mwenyekiti Idama Kabanzi diwani wa kata ya Nyanzeba na kuhudhuriwa na  madiwani, Wajumbe pamoja na mbunge  na viongozi mbalimbali wa halmashauri hiyo huku lengo likiwa ni kujadili ajenda mbalimbali za kutekeleza mikakati ya maendeleo katika halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho,  kwa upande wa sekta ya afya mbunge wa halmashauri ya wilaya ya Buchosa Dkt. Charles Tizeba ameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kujenga hospitali ya kisasa wilayani hapo ambayo inatarajia kuanza kutoa huduma ifikapo mwishoni mwa mwaka huu ambapo walengwa wakuu watakuwa akina mama wajawazito,  watoto pamoja na wananchi wote wa halmashauri ya wilaya ya Buchosa.

"Nipende kuishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutujengea hospitali hii ya kisasa ambayo inatarajia kuanza kutoa huduma ifikapo mwishoni mwa mwaka huu. " Alisema Tizeba.

Naye, Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Buchosa, Bw. Chrispine  Luhanda ameeleza kuwa hospitali hiyo itakapokamilika wananchi wa Buchosa ambao wengi wanakwenda kupata huduma ya afya sengerema na geita ambapo wanatembea umbali mrefu watakuwa  wamesogezewa huduma hiyo kwa ukaribu zaidi.

"Matarajio yetu ni kwamba baada ya hospitali hii kukamilika wananchi wa halmashauri ya Buchosa watakuwa wamesogezewa huduma hii ya afya kwa ukaribu,  sababu wamekuwa wakienda kupata huduma hiyo sengerema, geita na wengine kuvuka hadi Mwanza. "Alisema Luhanda.

Aidha, diwani wa viti maalumu halmashauri ya wilaya Buchosa, tarafa ya ya Nyehunge Ndg. Mwamini Antony Gandama ameshauri viongozi  hao kuweza kutembelea miradi wanayoisimamia ili kuleta tija na matokeo ya pesa zinazotolewa na serikali yaonekane kwa wananchi wa halmashauri hiyo.  

" Nipende kuwashauri viongozi kuweza kutembelea  miradi wanayoisimamia ili ilete tija na matokeo ya pesa zinazotolewa na serikali  yaweze kuonekana kwa wananchi wa Buchosa. " Alisema Gandama.

Katika hatua nyingine Eng. Kassian Mwitike, Meneja wa usambazaji maji  sengerema amebainisha kuwa wameshaweka mikakati mbalimbali kwa kushirikiana serikali na kupitia vyanzo mbalimbali kukamilisha mradi wa maji wa Nyakalilo na Bukokwa ulioanza mwaka 2014  ambao umeshafikia asilimia 90% ya utekelezaji wake na kusema  utakamilika ifikapo mwezi disemba mwaka huu ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

"Kwa mikakati tuliyojipanga kupitia wakala wa usambazaji maji na usafi wa mazingira vijijini,  serikali na kupitia vyanzo mbalimbali tumejipanga kuhakikisha mradi wa maji wa Nyakalilo na Bukokwa ambao umeshafikia asilimia 90% ya utekelezaji wake kukamilika ifikapo mwezi disemba. " Alisema Mwitike.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa kikao hicho Idama  Kabanzi amewaomba wakurugenzi na viongozi wote kuhakikisha wanakaa kwenye nafasi nzuri ya kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili halmashauri ya Buchosa ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na changamoto hizo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.