• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wahujumu Pembejeo za kilimo Wakamatwa Mwanza

Posted on: May 8th, 2020

Mhasibu wa AMCOS ya MHEDI iliyopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga na wafanyabiashara 13 na madalili 3  washikiliwa na TAKUKURU Mwanza kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa kinyume na sheria.


Akitoa taarifa hiyo Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mwanza Emmanuel Stenga alisema Mhasibu Paulo Nkuba alikuwa akisafirisha na kuuza dawa za kilimo zilizonunuliwa na serikali na kupelekewa Bodi ya pamba kwa lengo la kuwapatia wakulima wa pamba kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa madalali na wafanyabiashara wa maduka ya pembejeo za kilimo maeneo ya Lumumba Jijini hapa .

Alisema TAKUKURU ilifanya upekuzi kwenye madauka ya bembejeo za kilimo baada ya kupata taarifa kutoka bodi ya pamba na kubaini kuwa dawa hizo zenye thamani ya shillingi 12,609,000 zimeuzwa kwa wafanyabiashara hao kinyume na utaratibu .

"Baada ya kubaini changamoto hiyo tumefanya ufatiliaji na kutambua kwa nini pembejeo za kilimo haziwafikii wakulima kwa wakati kumbe kuna baadhi ya viongozi wa AMCOS wasio waadilifu wamekuwa wakiyauza madawa hayo kwa njia ya rushwa pia tumefatilia na madeni ya wakulima wa AMCOS na tumeweza kuokoa fedha nyingi ambazo zimehujumiwa na baadhi ya viongozi mbalimbali mkoani hapa"alisema Stenga.

Aliongeza kuwa baadhi ya viongozi hao wamekuwa wajizifanyia hujuma fedha za serikali kwa kuandaa vocha za usambazaji wa pembejeo hizo na kudai fedha nyingi serikali sambamba na kuwakata fedha wakulima na kutoziwasilisha serikalini pamoja kuwauzia wafanyabiashara badala ya wakulima.

Alisema watuhumiwa wote wamekwenda kinyume na kifungu 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11/2007 pamoja na kupatikana kwa mali njia isiyo halali kinyume na kifungu cha 311 cha sheria ya kanuni ya adhabu na marekebisho yake ya mwaka 2002 hivyo uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea kwa kuwabaini wote wanaohusika na ubadhirifu huu pindi uchunguzi utakapokamilika wahusika wote watafikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma ziazowakabili.

Aliongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na hawatovumilia kuona upotevu wa fedha za serikali pia waliwataka wafanyabiashara wote kuacha tabia hiyo vinginevyo hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kuhusika na ubadirifu wa pembejeo za kilimo ,aidha wakulima watoe ushirikiano kwa TAKUKURU pindi wanapoona mambo hayaendi kwa utaratibu uliokusudiwa.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa huo Mhe.John Mongella baada ya kupokea taarifa hiyo alisema tumeona pembejeo zilizokamatwa ambazo ni ruzuku ya serikali zinazotakiwa kwenda kwa wakulima moja kwa moja kwa sababu kuna kodi ya wananchi ilipelekwa humo ili kuinua sekta hiyo lakini baadhi ya watu wasio na uzalendo wameamua kuzifanyia biashara pembejeo hizo.

Hivyo aliwataka watanzania kuwa wazalendo na kutoa ushirikiano pindi wanapoona viashiria vya rushwa vinapotokea.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.