• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

FAMILIA ZIIMARISHWE ILI KULINDA KIZAZI CHA WATOTO:RAS BALANDYA

Posted on: July 22nd, 2024

FAMILIA ZIIMARISHWE ILI KULINDA KIZAZI CHA WATOTO:RAS BALANDYA


Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu Bw.Daniel Machunda ametaka kuwepo na mipango endelevu ya elimu kwa familia ili ziimarishwe na kuwa Taasisi imara za malezi ya watoto na hatimaye kuwa na Taifa lililo staarabika.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa kwenye kikao kazi cha kutathmini malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia miaka 0-8 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Tanroad,Machunda amebainisha msingi imara wa malezi ya mtoto unaanzia ngazi ya familia na endapo eneo hilo kukiwa na ulegevu tabia ya mtoto inaanza kuharibikia hapo.

"Ndugu zangu washiriki wa kikao kazi hiki nawaombeni sana mkalifanyie kazi jambo hili,Dunia sasa imekumbwa na changamoto nyingi hasa mabadiliko ya teknolojia,vitendo vya ukatili pia na umasikini,mkazo wa elimu kwa familia ni lazima uzingatiwe",Machunda

Amesema bado familia nyingi haziwajibiki ipasavyo katika malezi ya watoto wao na badala yake wanatumia muda mwingi katika shughuli zao za kuzipatia kipato familia na kufanya mtoto kupitia hatua mbalimbali hatarishi.

Amewataka washiriki hao ambao ni Maafisa Lishe,Ustawi wa Jamii,Maendeleo ya Jamii na Mipango kuhakikisha wanakuwa wabunifu wazuri katika kuielimisha Jamii kuhusu umuhimu wa malezi ya mtoto.

"Mtoto anatakiwa kulelewa katika misingi mikuu kama kumjua Mungu kwa Imani yake ya dini,kuheshimu watu wakubwa,kupata elimu na kupata nahitaji ya msingi kama chakula,afya,ulinzi na malazi",amefafanua Machunda wakati akitoa mada kwenye kikao kazi hicho.

Mwakilishi kutoka Wizara  ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum anayeshughulikia dawati la mtoto Bi.Merry Shilla amesema kwa kutambua umuhimu wa malezi ya mtoto wamejipanga kuwajengea uwezo Maafisa wake wa ngazi zoto mikoani ili kuwepo na muendelezo mzuri wa malezi ya mtoto.

"Bado kumekuwa na vitendo vya ukatili kwa watoto na pia kukosa malezi imara kutoka kwa familia, hizi changamoto hatuna budi kukusanya nguvu kwa pamoja ili kukabiliana nazo",Shilla

Kikao kazi hicho kimewashirikisha Maafisa Ustawi wa Jamii,Maendeleo ya Jamii,Maafisa Lishe,Mipango na Waganga wakuu wa Wilaya kutoka Halmashauri zote 8 za Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.