• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI MWANZA WATAKIWA KUCHANGAMKIA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: January 30th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi mkoani humo kujiunga na huduma za bima ya afya kwa wote iliyozinduliwa kwa awamu ya kwanza na Waziri wa Afya Januari 26, 2026 ili kujihakikishia matibabu ya uhakika.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo tarehe 30 Januari, 2026 wakati akikagua ujenzi wa wodi ya wazazi katika kituo cha Afya cha Nyanguge kinachohudumia wananchi 22865 kutoka katika kata hiyo na kata jirani.

Mhe. Mtanda amesema ukamilifu wa wodi hiyo utasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi hivyo ni lazima Mkurugenzi Mtendaji akamilishe kwa haraka ujenzi wa wodi hiyo kwa kuongeza pia fedha kiasi cha Tshs. Milioni 50 kwani serikali imeleta Milioni 200.

“Serikali imezindua mpango wa bima ya afya kwa wote, naomba liwepo dawati la huduma za bima ya afya ili wasihangaike na zile kero za wagonjwa kuomba msamaha au wakati wa kuwatoa ndugu zao waliofariki ziishe. “ Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amewataka viongozi wa Mwanza kukamilisha taratibu za uanzishwaji wa eneo la uwekezaji ili lianze kazi kwani litainua uchumi wa wananchi wa mkoa wote wa Mwanza na akatoa wito kuepuka migogoro wa ardhi wakati wa utekelezaji wa mradi.

“Nataka niwaambie watu wa Magu, mkitaka mafanikio basi eneo la Viwanda la Matela B katika kijiji cha Matela ni lazima mulichagamkie kwa kukaa na wawekezaji kuona namna ya kufikia muafaka kwenye upimaji na uchukuaji wa maeneo kwa wanaanchi bila kusababisha migogoro.” Mhe. Mtanda.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema bima ya Afya kwa wote inatoa fursa ya kuunganishwa watu 6 kutoka kwenye Kaya kwa Tshs. 150,000 ambao watapata huduma kuanzia ngazi za zahanati hadi rufaa mkoa na hivi karibuni uandikishaji unaanza.

Ameongeza kuwa bima ya afya kwa wote inajumuisha huduma 372 kwa kiasi hicho tu cha fedha na inatoa fursa kwa matibabu ya upasuaji, madawa na hata huduma za dharula na kwamba inatoa fursa kwa wategemezi kuhudumiwa ndani ya kifurushi cha kaya ya watu sita tofauti na hapo awali.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NYANZA YATAKIWA KUHAKIKISHA PEMBEJEO ZA PAMBA ZINAWAFIKIA WAKULIMA KWA WAKATI

    January 30, 2026
  • WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KUKUZA UCHUMI

    January 30, 2026
  • USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO UNAHITAJI UWAJIBIKAJI WA PAMOJA

    January 30, 2026
  • WANANCHI MWANZA WATAKIWA KUCHANGAMKIA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 30, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.