• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HADI KUFIKA DISEMBA TUNATARAJIA KUTOA CHANZO KWA WATOTO WA KIKE ZAIDI YA MILIONI 4 : WAZIRI UMMY

Posted on: April 22nd, 2024

HADI KUFIKA DISEMBA TUNATARAJIA KUTOA CHANZO KWA WATOTO WA KIKE ZAIDI YA MILIONI 4 : WAZIRI UMMY


Waziri wa Afya Mhe: Ummy Mwalimu (MB) leo Aprili 22, 2024 amezindua rasmi Maadhimisho ya wiki ya chanjo Kitaifa ya Saratani ya mlango wa kizazi kwa watoto wa kike kuanzia miaka 9-14 na kusema mpango wa Serikali hadi kufika Disemba mwaka huu wanatarajia kufikia idadi ya watoto zaidi ya milioni 4.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Mkoani Mwanza katika viwanja vya Furahisha, Mhe. Ummy amesema Maadhimisho yanakwenda kwa kutoa dozi mara moja tu tofauti na hapo awali walitoa dozi mara mbili na hii ni kutokana na utafiti wa kitaalamu uliofanywa hapa nchini na baadaye kuridhiwa na Shirika la Afya Duniani WHO.

"Tanzania ni ya nne Duniani kwa tatizo hili la Saratani ya shingo ya kizazi, takwimu zinaonesha katika wagonjwa 100 wa Saratani, 25 wana tatizo la Saratani ya shingo ya kizazi tuna wajibu wa kutokomeza hali hii na tuepuke upotoshaji wowote wa chanjo hii", Waziri Ummy.

Amesema Serikali ina nia njema ya kuhakikisha Taifa linakuwa salama na lenye watu wenye afya bora,ndiyo maana chanjo hii ni bure na haihusiani na uzazi wa mpango kama baadhi wanavyodhania.

"Nawasihi sana nyie wanangu mliopo hapa epukeni ngono kabla ya wakati wake,wengi wenu mnapata tatizo hili kutokana na kuyakimbilia haya mambo mapema na matokeo yake mnaingia katika gharama kubwa ya matibabu ya saratani,"amesisitiza Waziri wa Afya.

Aidha amewataka wazazi kuiunga mkono Serikali katika wiki hii ya kampeni kwa kuhakikisha watoto hao wanapata chanjo itakayo muweka salama katika maisha yake.

Awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe:Amina Makilagi aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa ameishukuru Serikali kwa kuleta miradi ya Afya yenye gharama ya zaidi ya shs bilioni 48 na kumuhakikishia Waziri Ummy miradi hiyo itasimamiwa kikamilifu na kukamilika kwa wakati ili iwe na tija kwa wananchi.

"Mhe: Waziri tuna vituo 400 vinavyotoa chanjo Mkoani hapa na  Machi 2024 tumetoa chanjo kwa watoto 37213,na wiki hii ya kampeni tutahakikisha tutazingatia maelekezo yote ya Serikali ili kutimiza malengo ya kuwa na Taifa lenye watu salama," Mhe:Makilagi

Mdhibti  ubora wa shule kanda ya ziwa Bi.Lucy Nyanda amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha malengo ya kufaniikisha kampeni ya chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi inafanyika kwa ubora na kwa walengwa wote.

"Wazazi wenzangu naomba tuelewane katika hili jambo tujiepushe na maneno ya upotoshaji kuhusiana na kampeni za chanjo,tuendelee kuelimika na kuzingatia maelekezo yote sahihi yanayotolewa na Serikali",Mdhibti ubora.

Kila mwisho wa jumla la Aprili Tanzania inaungana na Mataifa Duniani katika Maadhimisho ya chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.