• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara,Rai ya ujenzi wa Taifa imara yatolewa Mwanza

Posted on: December 9th, 2022

*Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara,Rai ya ujenzi wa Taifa imara yatolewa Mwanza.


Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara yamefanyika leo nchini huku Rai ya kuthamini amani na umoja na kulijenga Taifa kiuchumi ikihimizwa kwa Watanzania.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana akizungumza katika maadhimisho hayo Wilayani Magu amesema  hakutakuwa na maana kama tunafanya maadhimisho haya huku amani miongoni mwa Watanzania ikiwa hakuna ni dhahiri Taifa haliwezi kuwa na Maendeleo yoyote.

Amesema Nchi yetu imebarikiwa kuwa na amani na umoja ulioasisiwa na Viongozi wetu Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere na Abeid Karume na tumeendelea kuona maendeleo ndani ya Taifa letu tangu Uhuru hadi sasa.

"Wakati wa miaka ya Uhuru Mkoa wa Mwanza ulikuwa na shule za Sekondari 5 lakini sasa tunazo 317,Hospitali zilikuwa 3 za Wilaya lakini sasa tunazo 26 wakati huduma ya maji ilikuwa inawafikia watu kwa asilimia 19 lakini sasa ni asilimia 60 Wananchi wanapata rasilimali hiyo" amesema Mtendaji huyo Mkuu wa Mkoa.

Amewakumbusha wananchi kuendelea kuwaenzi kwa vitendo Viongozi wetu waliopigania Maendeleo ya Taifa hili kwa kufanya kazi kwa bidii,ubunifu na kutanguliza uzalendo.

"Tunaona kasi ya maendeleo inayofanywa na Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan,kila mwananchi ana kila sababu ya kuunga mkono jitihada hizi ambazo ni kwa faida yetu na vizazi vijavyo"amesisitiza Ndg.Balandya

Awali akitoa salamu za Wilaya ya Magu Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Salum Kalli amesema Miradi mingi katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya afya na shule imetokana na uimara wa Serikali ya awamu ya Sita ambayo imeonesha kwa vitendo dhamira ya kumletea maendeleo mwananchi.

Maadhimisho hayo yaliyokwenda pamoja na Mdhahalo uliolenga tumetoka wapi,tulipo sasa na tunakwenda wapi tangu kupata Uhuru wa Tanzania Bara,"Tujifunze kutanguliza uzalendo,kuepuka tamaa na kuridhika na kipato halali,kwa kufanya hivyo tutaepuka rushwa na kujenga Taifa lenye weledi"Mchungaji Dkt.Jacob Mutash.

"Tujenge utamaduni wa kuwapenda Viongozi wetu,tuwakosoe kwa busara na kuepukana na siasa za kusigana na chuki tukizingatia haya tutazidi kuwaenzi kwa vitendo waasisi wetu ambao miongozo yao imezidi kutuimarisha siku hadi siku"Padri John Kasembo mwalimu na mshauri wa viongozi.

Tanzania Bara imepata Uhuru wake Disemba 9 1961 kutoka kwa mkoloni Muingereza,huku kila mwaka yakifanyika maadhimisho hayo kwa kushiriki shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.