• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza wapongezwa kwa utayari na tishio la ugonjwa wa Ebola

Posted on: September 29th, 2022

Wizara ya Afya imeridhishwa na utayari kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa ukiwemo Mwanza kuhusiana na ugonjwa wa Ebola ambao umetokea huko nchini Uganda na kuhimiza elimu kwa umma itolewe ili Wananchi wapate ufahamu wa kutosha kuhusiana na ugonjwa huo.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi akizungumza leo na vyombo vya habari kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amesema amefanya ziara Mikoa ya Kagera na Mwanza kujionea hatua zilizochukuliwa kwa tahadhari ya ugonjwa huo na kuridhika huku akitaka Wataalamu wote wa afya kujikita kutoa elimu kuanzia mtaani na kwenye vyombo vya Habari.

"Niwafahamishe Wananchi nchi yetu ipo salama hakuna mgonjwa yoyote aliyegundulika hadi sasa lakini tusibweteke na badala yake tuelimike vyema na kujenga utamaduni wa kunawa mikono mara kwa mara kwani ugonjwa wa Ebola unaambukizwa kwa njia ya vimelea vya maji na damu" amesema Katibu Mkuu.

Mtendaji huyo Mkuu kutoka Wizara ya Afya amewataka Wataalamu wa Afya waliopo kwenye Viwanja vya Ndege na Bandari kuongeza umakini na usahihi wa taarifa za wanaoingia na kutoka kupitia mifumo ya kisasa ili kuudhibiti ugonjwa huo.

Kwa upande wake kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw Daniel Machunda akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoani humo Balandya Elikana, amemuhakikishia Profesa Makubi kuwa Mkoa wa Mwanza umeyapokea na kuyafanyia kazi maelekezo yote kutoka Wizarani ili Wananchi waendelee kubaki salama.

"Mara baada ya kutokea visa vya ugonjwa wa Ebola  nchini Uganda Mwanza tulianza kuchukua tahadhari mara moja kwa kutenga vituo vya kuwapokea wagongwa watakaogundulika na kuhakikisha vifaa vyote muhimu vipo tayari" Kaimu Katibu Tawala.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt Thomas Rutachunzibwa amebainisha kuwa  kwa kutambua hatari ya ugonjwa wa Ebola kila Halmashauri imetenga Vituo vya kuwapokea wagonjwa watakaobainika.

"Hapa Mwanza mjini tuna vituo vitatu vya Buswelu, Mkuyuni pamoja na Hospitali ya Mkoa ya Rufaa Sekou Toure pia Hospitali ya Kanda ya Bugando ipo tayari endapo itatokea visa vya ugonjwa huo" amesema Mganga Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Dkt. Rutachunzibwa amesema wametoa elimu ya kutosha kwa Wataalamu wote wa afya ili kuhakikisha wanakuwa salama endapo itatokea hali ya kumhudumia mgonjwa wa Ebola.

Miongoni mwa dalili za ugonjwa wa Ebola ni homa kali, mwili kuchoka bila sababu, kutokwa na damu kwenye matundu yote ya mwili, kuharisha na kupoteza fahamu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.