• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Nyamagana Yaahidi Milioni 200 kwa Vikundi

Posted on: August 9th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Dtk. Philis Mishack Nyimbi ameahidi kutoa millioni 200 kwa wafanya biashara wadogo wadogo  ili waweze kujiongezea mitaji  na kuendelea kuchangia uchumi wa nchi.

Mhe.Dkt.Nyimbi ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi katika soko kuu la Mwanza pamoja na wafanyabiashara wadogo wadogo aliowakuta katika eneo hilo.

"Naahidi kutoa cheki ya millioni 200 kwa wafanya biashara wadogo wadogo na wajasiliamali ambapo fedha hiyo inatoka Halmashauri ya jiji la Mwanza  na itagawiwa kwa vikundi mbalimbali vya kina mama, vijana na walemavu hivyo itasaidia kuleta  maendeleo katika jamii," alisema Mhe. Dkt.Nyimbi.

Hata hivyo Mhe.Dkt Nyimbi aliongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa na Wilaya kama Sehemu ya kujitambulisha kwa wananchi na kutembelea  miradi mbalimbali ya maendeleo.

Naye Mhe. Mongella katika ziara hiyo amesisitiza swala la usafi,usalama pamoja na kufanya kazi kwa juhudi kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuondoa maisha magumu kwa wananchi na kuongeza kipato cha familia na nchi kwa ujumla.

"Nahitaji ushirikiano kutoka kwenu zaidi, pia nawapongeza wamachinga kwa kuleta amani na utulivu kwenye jiji letu la Mwanza kwa kupunguza uhalifu kwani mnatupa ushirikiano mkubwa, hata hivyo nahitaji zoezi la usafi la kila Jumamosi liendelee ili kuepuka ugonjwa wa kipindupindu.

Aidha ameongeza kuwa kwa kuendeleza kauli ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kila mtu ajitume kwa nafasi yake na kufanya kazi kwa bidii kwani Mhe.Rais anasema "Hapa kazi tu."

Mhe. Mongella aliwasisitizia swala la kulipa kodi kwa kila mfanya biashara hata kama ni kiasi kidogo kwani kwa kufanya hivyo wanachangia maendeleo ya nchi.

 Mhe. Mongella  alitembelea pia shule ya Nyakato B  na kuongea na wanafunzi ambapo amewasisitiza kusoma kwa bidii ili kuweza kufikia malengo yao na alitoa zawadi ya fedha kwa wanafunzi wa darasa la kwanza na la tatu waliojibu  maswali yake kwa ufasaha ili kununulia madaftari na kalamu.

Hata hivyo kamati ilimalizia ziara hiyo kwa  kutembelea  Zahanati ya Isebanda, Wasambazaji wa dawa  za kilimo na mifugo( Twiga Chemical Industries),  pamoja na Shule ya Nyakato B.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.