• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO UTEKELEZAJI WA MIRADI SENGEREMA

Posted on: July 30th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana akiwa ameongozana na wajumbe wa Kamati ya Usalama Mkoa pamoja na Wakuu wa Idara kutoka Sekretarieti ya Mkoa amefanya ziara wilayani Sengerema kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Akiongea katika mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya sekondari katika kijiji cha Isungang’holo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema kuhakikisha huduma za msingi kama Umeme shuleni hapo pamoja na kuweka uzio na kupanda miti ili kutunza mazingira.


Aidha, ameiagiza kamati ya ujenzi wa shule ya msingi Nyanango (Buchosa) pamoja na Isungang’holo kusimamia unadhifu wa mazingira ya shule hiyo kwani serikali imewekeza zaidi ya Tsh. Milioni 580 ili kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora hivyo hawana budi kuenzi juhudi hizo.

Akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Sima, Katibu Tawala amewahakikisha wakazi hao huduma ya maji safi siku za usoni kutokana na mradi mkubwa wa maji unaojengwa kwa zaidi ya Tshs. Bilioni 3 pamoja na changamoto kadhaa zilizochelewesha mradi huo kutokamilika mwaka 2023 sasa zimeshashughulikiwa.


Halikadhalika, ameiagiza Halmashauri hiyo kukamilisha ujenzi wa madarasa yanayojengwa katika shule ya msingi Nyasenga Nyampande pamoja na kuhakikisha wanaweka mitaro ya maji katika ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka CCM hadi katikati ya mji wa Sengerema.

Akikagua huduma za Afya wilayani humo, Bw. Balandya ameitaka Halmashauri ya Sengerema kukamilisha nyumba ya familia mbili inayojengwa katika Zahanati ya Butunga pamoja na Buchosa kuharakisha ujenzi wa Zahanati katika kijiji cha Nyabutanga ili wananchi wapate huduma za afya jirani na makazi.


Vilevile, Katibu Tawala amewaagiza RUWASA kusanifu na kupanua upya mradi na kuhakikisha wanapeleka huduma ya maji safi kwenye vitongoji vya Itabagumba, Mbugani na Bulyaheke A na B kupitia mradi wa zaidi ya Tshs. Bilioni 3 unaotekelezwa katika kijiji cha Kazunzu kabla ya kupeleka maji hayo katika maeneo ya mbali.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA WAASWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KUFANYA KILIMO CHA KISASA

    August 02, 2025
  • RMO MWANZA AONGOZA ZIARA YA MAFUNZO YA USAFI NA MAZINGIRA MKOANI IRINGA

    July 21, 2025
  • RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO UTEKELEZAJI WA MIRADI SENGEREMA

    July 30, 2025
  • UIMARISHWAJI WA MIFUMO YA KIELETRONIKI IMEONGEZA UWAJIBIKAJI – RAS BALANDYA

    July 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.