• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZIASA NG'O KULINDA MAADILI YA KITANZANIA

Posted on: August 16th, 2023

RC MAKALLA AZIASA NG'O KULINDA MAADILI YA KITANZANIA


Atoa wito kufanya kazi kizalendo na kwa uwazi


Ayaagiza mashirika hayo kufuata sheria za nchi na kuwa tayari kukaguliwa


Amewasihi kufikisha huduma kwenye maeneo ya vijijini


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kufanya kazi kwa kufuata sheria za nchi na kulinda mila, tamaduni na desturi ili kujenga jamii yenye maadili.

Ametoa wito huo leo wakati wa kilele cha Mkutano/Jukwaa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Mwanza lililofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

CPA Makalla amesema mashirika yasiyo ya Serikali ni nguzo muhimu katika kujenga uchumi wa nchi lakini wanapaswa kuenenda kwa kufanya shughuli kwa mujibu wa usajili wa taasisi zao.

"Mashirika yasiyo ya Kiserikali ni wadau muhimu wa maendeleo nchini na ndio maana hata kwenye Bajeti ya Serikali  utasikia eneo la wafadhili nami nawapa ahadi ya ushirikiano wakati wote maana hata kwenye mabanda nimeona mnajihusisha na huduma muhimu za kijamii kama Elimu na Afya."Makalla.

Aidha, amewaahidi kupokea ushauri wa aina yoyote kutoka kwenye mashirika hayo huku akibainisha kuwa wao wana nafasi kubwa zaidi ya kuona kinachoendelea kwenye jamii na akatoa wito kwao kuhakikisha wanafikisha huduma kwenye maeneo ya vijijini.

Musa Sang'anya, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali amefafanua kuwa jukwaa hilo lilizinduliwa na Rais Samia na kwamba ni mwaka wa pili mfululizo linafanyika na mwezi Oktoba Makamu wa Rais atakua Mgeni Rasmi kwenye kilele kitakachofanyika jijini Dodoma kitaifa.

Katibu Mkuu Baraza la Taifa la Mashirika  yasiyo ya Serikali Revocatus Sono ameyataka mashirika hayo kufuata sheria na kanuni kama zinavyoelekezwa na sheria namba 24 ya mashirika yasiyo ya Serikali ya mwaka 2002.

Janeth Shishila Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mwanza ambaye ni Msajili msaidizi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali mkoa wa Mwanza ametumia wasaa huo kuzitaka asasi hizo kutoa taarifa ya shughuli wanazofanya mkoani humo ili serikali iweze kutambua mchango wao mkoani humo.

Jukwaa hilo la siku mbili Mkoa wa Mwanza limechagizwa na Kaulimbiu isemayo Mashirika Yetu,  Maadili yetu, Taifa Letu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.