• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima afurahishwa na Benki ya NMB kujihusisha na kilimo

Posted on: December 1st, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima ametoa rai kwa benki ya NMB kuendelea kuchangia maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi nchini kupitia huduma za kifedha wanazotoa.

Akizungumza na Viongozi na Mameneja wa benki hiyo waliotoka kanda zote nchini leo Jijini Mwanza, Mhe. Malima amewapongeza kwa kubuni huduma mpya bora za kiushindani wanazozitoa kwa jamii kama zinazowanufaisha wajasiliamali wadogo.

Aidha, Mhe. Malima ameipongeza benki hiyo kwa kuendelea kuboresha huduma zao kwenda kwenye mifumo ya kidigiti siku hadi siku kwani kwa maendeleo ya sayansi na teknolojia jambo hilo haliepukiki kutokana na ushindani wa kibenki.

"Faraja yangu kubwa kwenu ni kuona mnajihusisha na Sekta ya Kilimo tena katika nyanja zote za mifugo, uvuvi na ufugaji wa Nyuki sehemu ambazo wananchi wengi wanaendesha maisha yao huko" Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, ametoa wito kwa benki hiyo kuborsha huduma za mikopo kwa wajasiliamali na vikundi vya wananchi wanaojihusisha na shughuli ndogondogo za kujitafutia kipato kwa kuweka masharti mepesi kwani wananchi wengi wa kipato cha chini lakini wamekua wakikosa mitaji.

Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dkt. Edwin Mhede amesema Benki hiyo ina mikakati ya kuwafikia wananchi kupitia uwajibikaji wao kwa jamii kwa kuwa sehemu ya Maendeleo yao kwa kuiunga Mkono Serikali kusaidia kwenye utoaji wa huduma mbalimbali kwa kusaidia vifaa kwenye Sekta ya Maji, Elimu na Afya.

"Benki yetu ilianzishwa mwaka 1997 na wakati huo tulikua na Matawi 97 tu nchini lakini sasa tumefikisha 228, tulikua hatuna mifumo ya digitali lakini hivi sasa tuna mifumo mbalimbali na tunashukuru sana Serikali, Wadau na Wateja wetu kwani wametupa faida kubwa hadi kufikia Bilioni 321 baada ya kodi ndani ya robo tatu tu za Mwaka." Kaimu Mtendaji Mkuu NMB,  Filbert Mponzi.

Mkutano huo wa Benki ya NMB umewakutanisha Viongozi na Mameneja zaidi ya 250 kutoka kanda zote nchini wakisherehekea kwa pamoja kuwa na tuzo 18 ndani ya mwaka mmoja kwa utoaji wa huduma mbalimbali kwa ubora mkubwa kutokana na kufanya Biasha kwa ufanisi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.