• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AFANYA KIKAO NA NAIBU WAZIRI TAMISEMI (AFYA)

Posted on: December 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Desemba 16, 2025 amefanya kikao kifupi na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia Afya, Mhe. Dkt. Jafar Rajab Seif, ambaye yupo mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya sekta ya afya katika Wilaya za Ilemela na Nyamagana.

Kikao hicho kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa kimejadili maendeleo ya huduma za afya katika mkoa huo, na kujadili mikakati ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na changamoto zinazokabiliwa na sekta hiyo.

Mhe. Dkt. Rajab Seif amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu katika kuhakikisha kwamba miradi ya afya inatekelezwa kwa ufanisi na inawanufaisha wananchi.

“Ziara yangu hapa Mwanza ni sehemu ya juhudi zetu za kuhakikisha kwamba huduma za afya zinaboreshwa na zinazifikia jamii kwa wakati. Tutaendelea kutoa kipaumbele katika maeneo ya afya ili wananchi wa Mwanza na maeneo mengine ya nchi wafaidike na huduma bora,” amesema Mhe. Dkt. Rajab Seif.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda ameeleza kuridhishwa kwake na hatua ambazo tayari zimechukuliwa katika kuboresha huduma za afya katika mkoa wake.

Aidha amemshukuru Mhe. Naibu Waziri kwa kutembelea Mkoa huo na kuahidi kuendelea kushirikiana katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya afya.

Ziara ya Mhe. Dkt. Jafar Rajab Seif imejumuisha ukaguzi wa vituo vya afya na hospitali katika wilaya za Ilemela na Nyamagana, ambapo amekutana na viongozi wa sekta ya afya pamoja na watumishi wa afya kwa lengo la kubaini changamoto na kujadiliana kuhusu njia za kutatua matatizo yanayojitokeza katika utoaji wa huduma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AFANYA KIKAO NA NAIBU WAZIRI TAMISEMI (AFYA)

    December 16, 2025
  • WAHITIMU WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA WANATEGEMEWA SANA NA SERIKALI- MHE. WANU

    December 15, 2025
  • WAKUU WA VITENGO MIKOA WATAKIWA KUTEKELEZA MIRADI KIZALENDO ILI KUCHOCHEA MAENDELEO

    December 12, 2025
  • WAZIRI ULEGA AWASILI MWANZA KUTEKELEZA AGIZO LA PM UKAGUZI MADARAJA

    December 11, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.