• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA ULIPAJI KODI, UWAJIBIKAJI NA AMANI

Posted on: December 24th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA ULIPAJI KODI, UWAJIBIKAJI NA AMANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amewataka viongozi wa Chama na Serikali kuhimiza na kusimamia ulipaji kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Ametoa agizo hilo leo Disemba 24, 2024 wakati akihitimisha kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa huku akisisitiza kuwa ili serikali iweze kutoa huduma bora kwa wananchi na kuwaletea maendeleo ni lazima iwe na fedha.

"Machafuko tunayo yashuhudia hivi sasa ulimwenguni baadhi yanatokana na hasira za wananchi kukosa huduma za msingi huku Serikali ikikosa fedha kutokana na kushindwa kukusanya kodi", Mhe. Mtanda.

Aidha, amewaomba viongozi kushirikiana kuhakikisha nidhamu ya ulipaji kodi inakuwepo na Serikali kuendelea na mkakati ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Akizungumza kuhusu uwajibikaji Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watumishi kuweka mbele nidhamu ya uwajibikaji kwa wananchi na kuepukana na vitendo vya rushwa.

"Viongozi wote mliopo hapa mkiwemo wakuu wa Wilaya na Taasisi kasimamieni hili msimuonee mtu aibu kumchukulia hatua, wananchi wana Imani na Serikali hii ya kuwapa huduma bora",amesisitiza Mtanda wakati wa kuhitimisha kikao hicho.


Hali kadhalika, amehimiza amani na hasa katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka kwa kuwataka wananchi kuwa watulivu na kuepukana na aina yoyote ya uvunjivu wa amani huku dola likiwa makini wakati wote kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao.

Katibu Tawala Mkoa wa

Mwanza Ndg. Balandya Elikana akijibu hoja ya mbunge wa Ilemela Mhe. Anjelina Mabula kuhusu ulipwaji wa fidia kaya 300,000 waliopisha maeneo yao kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege, amesema mchakato wote umekamilika kinachosubiriwa ni mrejesho kutoka mamlaka husika.

Kikao hicho cha Kamati ya Ushauri Mkoa kimepokea hoja ya Jimbo la Magu kugawanywa sehemu mbili na kuwepo Jimbo lingine la Sanjo kutokana na ukubwa na idadi ya wananchi zaidi ya laki nne huku hoja ya Jimbo la Sengerema kugawanywa na kuwepo na Jimbo la Karumo likitolewa maelekezo ya kufanyika kikao cha kitaalamu kabla ya kuwasilishwa kikao kijacho cha RCC.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.