• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA MUONGOZO NGUVU YA MALEZI NA UMUHIMU WA WAZAZI WOTE WAWILI KATIKA MAISHA YA MTOTO

Posted on: September 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesisitiza kuwa malezi bora ya mtoto hayawezi kufanikishwa na mzazi mmoja pekee, akibainisha kuwa ushirikiano wa karibu kati ya baba na mama ni nguzo muhimu katika kuhakikisha makuzi ya mtoto mwenye maadili, ujasiri na mafanikio ya baadaye.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo Septemba 19, 2025 alipokuwa katika Mahafali ya Kwanza ya Darasa la Saba na maonesho ya sayansi na ubunifu katika shule ya NEBRIX iliyopo Mtaa wa Chabakima Kata ya Shibula Wilaya ya Ilemela.

Mkuu huyo wa Mkoa ameeleza kuwa changamoto nyingi zinazowakumba watoto wa kizazi hiki zinachangiwa na ukosefu wa mshikamano wa kimalezi kati ya wazazi wawili, hali inayowafanya watoto kulelewa katika mazingira yasiyo na mwongozo thabiti.

“Siku hizi eti kuna Wazazi wanajiita single mothers, uongo mtupu, malezi ni ya wazazi wote wawili”.

Lakini pia Wazazi wa Kiume wamekuwa na shughuli nyingi wakisingizia wanatafuta pesa, sasa unakuta hawaweki dhamana ya kuwa karibu na watoto na mwisho wa siku fedha hawapati na ukaribu wa watoto haupo. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Mtanda ameeleza ni lazima Wazazi wote wawili kushirikiana katika kufuatilia mienendo na tabia za watoto ili kuwajengea msingi imara wa maisha yao ya baadae na kutatua changamoto zao wanapokumbana nazo kwa haraka ili wasikumbane na vishawishi.

“Mkiwa karibu na Watoto wenu mnaleta bondi, msipofanya hivyo upendo hauji, na ndio maana Wazazi wengi wanatekelezwa baada ya watoto wao kufanikiwa”. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa ametumia wasaa huo pia kuwataka Wazazi/Walezi kuhakikisha wanashiriki katika shughuli za uchaguzi mkuu kuanzia kampeni mpaka kushiriki zoezi la upigaji kura ifikapo Oktoba 29, 2025.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.