• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA PAMBA JIJI KUJA NA MATOKEO MAZURI LALA SALAMA YA LIGI KUU

Posted on: January 29th, 2025

RC MTANDA AWATAKA PAMBA JIJI  KUJA NA MATOKEO MAZURI LALA SALAMA YA LIGI KUU


Wakati filimbi ya lala salama ya ligi kuu ya NBC imepulizwa timu ya Pamba Jiji FC imetakiwa kuja na matokeo mazuri dimbani baada ya kufanyiwa maboresho ya kiufundi ikiwemo ingizo la wachezaji wapya na kuondolewa wale walioonekana ni mzigo kwa timu.

Rai hiyo imetolewa leo Januari 29, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni mlezi wa Pamba Jiji FC Mhe.Said Mtanda wakati wa hafla fupi ya chakula cha jioni aliyowaandalia timu hiyo kwenye ukumbi wa Gadh Hall na kusisitiza hakutakuwa na simile ya kuchukua maamuzi magumu itakapo bainika muhusika yoyote anaonesha dalili za kuiangamiza timu.

"Nawaomba katika hili tuelewane vizuri uongozi umetumia gharama kubwa ya kuiboresha timu wale tuliowaona siyo msaada kwa timu na kujiona wao ni wakubwa wa kuliko Pamba Jiji tumewaondoa,nawataka muanze kujitambua kwa kujituma uwanjani ili malengo yetu ya kubaki ligi kuu yatimie,"amesisitiza Mtanda wakati akizungumza na wachezaji na dawati zima la ufundi la timu hiyo.

Mtanda ambaye ni mpenda soka kindakindaki amekemea vikali baadhi ya wachezaji wanaojiingiza katika michezo ya kamali  na kusema huo ni utovu wa nidhamu usiyovumilika na hatua za kinidhamu zitamkuta yoyote atakaye bainika.

"Tayari kuna mmoja wenu nimempa onyo kali baada ya kumgundua kujihusisha na huo mchezo wa kijinga,nina uwezo wa hali ya juu wa kuwabaini narudia tena kuwaonya wacheni na wekeni mkazo uwanjani," mkuu wa Mkoa.

Aidha amelitaka pia dawati la ufundi chini ya kocha wake Freddy Felix Minziro kuwa chachu ya kufanya vizuri kwa timu hiyo kwani hata wao hawana uhakika wa kubaki salama endapo watakwenda kinyume na makubaliano yao kwenye mkataba.


Katika usajili wa dirisha dogo  uliofanywa na uongozi wa timu hiyo kwa ushauri wa kocha Minziro miongoni mwa wachezaji wapya ni pamoja na mshambuliaji Deus Kaseke.


Pamba Jiji FC iliyopo nafasi ya 14 na mtaji wa ponti 12 kibindoni itashuka dimbani Februari 5 mwaka huu kwenye uwanja wa Jamhuri kupepetana na wenyeji wao Dodoma Jiji FC ambao katika mzunguko wa kwanza walitoshana nguvu ya bila kufungana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.