• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza aendelea kutoa misaada Wanafunzi wa Sekondari ya Bwiru waliounguliwa na Bweni

Posted on: July 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo ameendelea kuongoza zoezi la kuwapatia mahitaji muhimu na ukaguzi wa ujenzi wa Bweni la Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Bwiru lililoungua wiki hii.

Akiwa Shuleni hapo Mhe Gabriel amewakabidhi Wanafunzi 76 Masanduku, Nguo, Makufuli na Shuka za kulalia ambayo ni michango inayoendelea kutolewa na Wadau mbalimbali wa Mwanza walioguswa na janga la moto huo.

"Naomba mtulie msiwe na shaka na badala yake ongezeni bidii ya masomo, tambueni Serikali ipo nanyi ndiyo maana mnaniona tangu siku ya ajali ya moto nipo hapa kuhakikisha kila kitu kinakaa sawa kama awali" Mkuu wa Mkoa.


Amesema ameridhishwa na kazi ya ujenzi wa Bweni na kuwataka Walimu wenye Taaluma ya Uhandisi kutoka Shule hiyo kushiriki ujenzi wa Bweni hilo na kuwahimiza wahusika wote kutanguliza uzalendo ili Wanafunzi hao wapate Bweni bora na la kisasa.

Katika hatua nyingine, Mhe Gabriel amefanya kikao kifupi na Walimu wa Sekondari ya Bwiru na kuwaahidi kuzitatua changamoto zao mbalimbali yakiwemo kuboresha nyumba zao za kuishi na mazingira ya kazi zao.

Baadhi ya Wanafunzi Michael Masatu na Shafii Said wakizungumza kwa niaba ya wenzao wamemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa msaada wa haraka walioutoa kwao mara baada ya Janga hilo la moto na kuahidi kusoma kwa bidii ili kutimiza malengo yao.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bwiru Thomas Werema amewaondoa shaka wazazi wa Wanafunzi na kusisitiza mazingira yote yapo salama na Wanafunzi wanaendelea na masomo vizuri.

Bweni la Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Bwiru liliteketea na moto siku ya Jumatano kuamkia Alhamisi na vitu vyote vilivyokuwemo   kuangamia na moto huo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.