• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SEKTA YA MADINI INAENDELEA KUKUA KWA KASI NCHINI : WAZIRI MAVUNDE

Posted on: January 5th, 2024

SEKTA YA MADINI INAENDELEA KUKUA KWA KASI NCHINI : WAZIRI MAVUNDE


Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amesema Sekta hiyo inazidi kukua ambapo 2022/23 Mauzo ya bidhaa za Madini nje ya nchi yalifikia 56% huku Mzunguko wa fedha ukichangia zaidi ya Trilioni 1.6 na zaidi ya Bilioni 678 zikikusanywa kama Maduhuli ya serikali zinazotokana na vyanzo mbalimbali vya mapato kwa zaidi ya Trilioni 2 ambayo ni 15% ya pato lote.

Mhe. Mavunde amebainisha hayo  mapema leo tarehe 05 Januari, 2024 kwenye Ukumbi wa Rock City Mkoani Mwanza wakati akizungumza na watoa huduma kwa wamiliki wa Leseni za Madini kwenye Mkutano uliowakutanisha wadau ili kujadili namna bora ya kuboresha sekta hiyo ili washiriki kwenye Uchimbaji waongezeke.

"Hadi sasa tumefanya utafiti kwa 16%  na lengo letu kubwa ni kubaini madini tuliyonayo na kuweza kujipanga ili kusaidia wananchi kuacha kufanya uchimbaji kwa kuhisi na hadi kufikia 2030 wananchi watakua wanajua hapa kuna nini kwa taarifa sahihi kutoka wizara ya Madini." Waziri Mavunde.

Vilevile, amebainisha kuwa wizara ya Madini ipo tayari kufanya maboresho ya kisheria ili kutoa fursa zaidi kwa washiriki kuweza kujihusisha na uchimbaji wa Madini nchini huku akitoa wito kwa taasisi za kifedha kuendelea kuwezesha mitaji ili watanzania wengi washiriki kwenye kuchimba na kuchangia rasilimali kwenye utoaji huduma kigodini.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameipongeza Wizara ya Madini kwa kufanya Utafiti wa kubaini ni eneo gani lina Madini ya aina gani na kwa kiasi gani kwani litasaidia kupunguza gharama za uendeshaji kwenye sekta hiyo nchini.

"Hakika Waziri Mavunde unafanya kazi nzuri kwa manufaa ya watanzania, ulipokua Naibu kwenye Kilimo ulifanya tafiti kuhusiana na Afya ya Udongo na huku kwenye Madini umekujq na jambo zuri la kubaini ni wapi kuna madini, ya aina gani na kwa kiasi gani, hapa utasaidia." Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amebainisha kuwa uwanja wa ndege wa Mwanza upo kwenye maboresho makubwa kuanza kuhudumia wasafiri na wasafurishaji wa Mizigo hivyo wadau wa sekta ya Madini watapata fursa ya kusafirisha bidhaa hizo kwenda nje ya nchi kwa ufanisi.

"Kutakua na Mgodi Mkubwa wa Madini ya Dhahabu wilayani Sengerema (Nyanzaga) ambao utashika nafasi ya Pili nchini ambao upo kwenye hatua mwisho kuanza kazi, nawaomba wanaMwanza mjiandae kunufaika na fursa." Makalla.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.