• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali Yazindua Ushoroba wa Kati kwenda Uganda

Posted on: July 30th, 2019


Serikali imezindua  na kutangaza rasmi uwepo wa fursa za   usafirishaji  mizingo kupitia Ushoroba wa Kati (central corridor) katika Bandari ya Mwanza Kusini kwenda nchi za Uganda na Sudani Kusini.

Uzinduzi huo umefanyika  eneo la Bandari ya Mwanza Kusini ambapo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe.Isack Kamwelwe amesema Serikali imefikia hatua ya kutangaza ushoroba wa kati kutokana na kuimarika kwa  mifumo ya njia kuu za usafirishaji wa anga, ardhi, barabara, reli ,mabomba, maji, mifumo takwimu na waya.


Mhe.Kamwelwe amesema utafiti uliofanywa na Serikali umebaini ushoroba wa kati ni miongoni wa shoroba zenye zaidi ya njia kuu tatu za usafirishaji na kufafanua kwamba usafirishaji kwa njia ya reli na meli ni usafiri wa uhakika na wenye gharama nafuu zaidi hususan mizigo inayosafirishwa kwa masafa marefu.


“Kwa takwimu  za Shirika la Chakula Duniani (WFP) zinaonyesha  kuwa kwa kutumia njia hii ya usafiri  huu unaokoa asilimia 40 ya fedha ikilinganishwa na gharama za kutumia njia mbadala.Usafiri wa reli na maji kupitia Ziwa Viktoria kwenda  Portbell Uganda umeunganishwa katika mfumo ambao treni inapowasili katika bandari ya Mwanza huingia moja kwa moja kwenye meli ya mizigi bila kushuka makasha.


“Ni jambo la kujivunia kwani ni nchi chache katika Afrika zenye miundombinu iliyounganishwa kwa utaratibu huu, kuanzia sasa mzingo unaposhushwa katika bandari ya Dar es Salaam unapakiwa kwenye treni ya shirika la reli nchini (TRC) na kuja Mwanza, unapofika hapa mzigo haushushwi bali mabehewa yanaingizwa moja kwa moja kwenye meli ya mizigo,”alisema.


Kamwelwe ameongeza kuwa hivi sasa Serikali kupitia kampuni ya meli inamiliki meli moja  ya mizigo inayoitwa MV Umoja yenye uwezo wa kubeba mabehewa 19 kwa wakati mmoja lakini kutokana na ongezeko la mahitaji na kwa kutambua umhimu wa kuwahudumia wananchi na nchi jirani,  imekusudia kujenga meli kubwa yenye uwezo wa kubeba mabehewa 50 kwa wakati mmoja sawa na tani 3000.


Amesisitiza kuwa  Serikali ya Tanzania na Uganda  tayari zimekubaliana kuweka utaratibu wa kuwa na kituo kimoja cha kufanya malipo kwa ajili ya mizigo ya kutoka Dar es Salaam, Mwanza hadi Portbell.


Amefafanua kuwa tangu utaratibu huo uanze kutumika Juni 24, mwaka huu  jumla ya mabehewa 1165 sawa na tani 45750 zimesafirishwa  kupitia ushoroba huo kwa njia ya reli na mali, kati ya mizigo hiyo mabehewa 874 sawa na tani  34,960 yalibeba mzigo wa WFP, hivyo shirika hilo la chakula limechangia asilimia 75 ya mizigo yote iliyosafirishwa kwa kipindi hicho.


Kwa upande wa Kiongozi wa WFP Tawi la Tanzania, Michael Dunford amesema uwepo wa shoroba ya kati umesaidia kupunguza gharama za kusafirisha vyakula kupitia Ziwa Viktoria ambapo kwa kuanzia Julai 2, hadi jana amesafiriksha mabehewa 18 kwenda Uganda kwa njia ya reli na maji.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella ametoa wito kwa wananchi, wafanyabiashara na taasisi kwa ujumla  kutoka Tanzania na nje ya nchi kutumia fursa ya uwepo wa shoroba ya kati  kupunguza gharama ya usafirishaji na hivyo kuinua vipato vyao.


 "Kuwepo kwa ushoruba huu kutachangia sana fursa ya uchumi kwa wana Mwanza na maeneo ya jirani watu wakiwa na uchumi unaoaminia na utulivu unakuwa mkubwa".alisema Mongella.


Pia alisema kuwepo kwa ushoroba wa kati ni fursa nyingine kwa mkoa wa Mwanza  kukuza uchumi wa mkoa, wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla ambapo alisisitiza  kwa uongozi wa mkoa utaendelea kuimarisha usalama wa watu na mali zao ili kila mmoja aweze kufanya shughuli zake kwa amani.


Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe.Mhandisi Robert Gabriel, Katibu Mkuu, Sekta ya Uchukuzi, Leonard Chamuriho na viongozi mbalimbali wa mashirika na taasisi za umma na binafsi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.