• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TIMU YA UFUATILIAJI MRADI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE YATINGA SITE

Posted on: February 8th, 2025

TIMU YA UFUATILIAJI MRADI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE YATINGA SITE


Tarehe 27 Desemba, 2024 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alimkabidhi Site Mkandarasi M/S Dimetoclasa Real Hope Ltd kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali yenye hadhi ya rufaa kwa Tshs. Bilioni 25 katika hafla ya kusaini mkataba iliyofanyika kwenye kijiji cha Bulamba.

Leo tarehe 08 Februari, 2025 timu ya ufuatiliaji ujenzi wa hoapitali ya rufaa ya Mkoa imetinga site (Site meeting 2) kwa ajili ya kufuatilia ujenzi wa hospitali hiyo ili kujiridhisha na kasi ya ujenzi pamoja na utekelezaji wa makubaliano ya matakwa ya mkataba kwa masilahi ya wananchi wa kisiwani humo.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya miundombinu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mhandisi Chagu Ng'homa amesema mpango wa Serikali ni kuanza kutoa huduma za afya mara moja pindi tu mradi utapokamilika kwa sehemu hiyo ya kwanza na ndio maana ujenzi umejumuisha majengo muhimu.

Amesema, jengo la ghorofa lenye uwezo wa kubeba vitanda 180, jengo la kuhifadhia maiti, kazi za nje na jengo la umeme pamoja na ofisi za walinzi ni sehemu ya majengo ya awali kutekelezwa na kwamba ndani ya siku 545 (Miezi 18) yatakamilika na huduma zitaanza kutolewa mara moja.

Katika kuhakikisha kasi ya ujenzi inaongezeka, Mhandisi Chagu akiwa kwenye ukaguzi wa eneo la ujenzi amepiga simu ya moja kwa moja kwa Mhandisi wa Wakala ya Umeme vijijini (REA) na kumtaka afike kwenye eneo hilo ili kuona namna ya kupeleka mradi wa umeme kwa ajili ya utekelezaji wa mradi

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jesca Lebba amesema sambamba na ujenzi huo taratibu zingine za kupata vifaa vya tiba na samani zinaendelea ili kuhakikisha mara tu ujenzi ukikamilika huduma za afya zinaanza kutolewa kwa wananchi wa Ukerewe.


Kwa upande wa mkandarasi, Mhandisi John Bhoke amesema shughuli za kuweka uzio kwenye eneo hilo zimekamilika, uondoaji wa udongo wa juu pamoja na kuandaa vipimo na eneo la jengo kuu la mradi zimeshakamilika na kwamba kwa sasa kazi inatakayofuata ni ujenzi wenyewe.

Aidha, ametoa wito kwa Mkandarasi mshauri pamoja na msimamizi wa mradi kuendelea kushirikiana na kuwasiliana mara kwa mara ili kupata uelewa wa pamoja wa kufanikisha ujenzi huo kwa ufanisi pamoja na kuhakikisha malipo hayachelewi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.