• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WADAU ZAO LA CHOROKO WAPEWA SOMO STAKABADHI GHALANI

Posted on: January 29th, 2025

WADAU ZAO LA CHOROKO WAPEWA SOMO STAKABADHI GHALANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefungua mkutano wa wadau wa zao la Choroko wenye lengo la kuelimishana umuhimu wa matumizi ya mfumo wa Stakabadhi Ghalani.

Akizungumza na wadau hao leo Januari 29, 2025 kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, Mtanda amesema mkutano huo ni muhimu kwani mfumo huo utakuwa ni mkombozi kwa mkulima  kwani ataweza kuuuza kwa bei nzuri na kuepukana na baadhi ya wajanja wachache wanaofaidika kwa ulaghai.

Mhe. Mtanda amebainisha huu ni mpango wa Serikali wenye nia njema ya kuhakikisha mkulima ananufaika na shughuli zake za shambani hivyo mazao ya jamii ya mikunde ambayo awali ilikuwa kama imesahaulika sasa iwe na tija kwao.

"Serikali imeunda Mamlaka ya udhibiti wa nafaka na mazao mchanganyiko COPRA lengo ni kuhakikisha kunakuwa na usimamizi mzuri wa mazao hayo kuanzia kilimo bora kitakacholeta uvunaji bora pia na bei nzuri kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani",amesisitiza mkuu huyo wa mkoa.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya udhibiti wa nafaka na mazao mchanganyiko COPRA, Irene Mlola amesema katika mfumo huo wataanza na mazao ya makundi matano ambayo ni nafaka ukiwemo mpunga na Mahindi,mbegu za mafuta ikijumuisha alizeti,michikichi, na ufuta,jamii ya bustani ni pamoja na maua na mbogamboga,jamii ya mikunde itajumuisha choroko,mbaazi,dengu na soya  na jamii ya mizizi ni viazi,mihogo na magimbi

Aidha kaimu Katibu tawala msaidizi uchumi na uzalishaji Innocent Keya akizungumzia uzalishaji wa zao la Choroko mkoani Mwanza amebainisha kwa msimu wa mwaka 2023-24 Mkoa umevuna tani 16,862.

"Msimu huu wa Masika Mkoa wa Mwanza utakuwa na mvua za wastani hadi chini ya wastani,wilaya za Kwimba,Magu,Misungwi na Sengerema zinazolima kwa wingi Choroko zitakuwa na mvua za milimita 350 hadi 400  ni vizuri wakulima wafahamu na kuzingatia taarifa hii ili wajipange vizuri,"Agustino Nduganda,mtaalamu kutoka Mamlaka ya hali ya hewani,TMA

Katika kikao hicho wadau wa mkutano huo ambao ni wenyeviti wa Halmashauri,wakuu wa wilaya wakulima,  na wasambazaji wameitaka COPRA kuendelea kuufanyia utafiti mzuri mfumo wa Stakabadhi Ghalani kabla haujaanza kutumika rasmi mkoani Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.