• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BARABARA MPYA YA LAMI KUCHOCHEA MAENDELEO KATA YA KIRUMBA-ILEMELA

Posted on: July 14th, 2023

*BARABARA MPYA YA LAMI KUCHOCHEA MAENDELEO KATA YA KIRUMBA-ILEMELA*


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023   Ndugu Abdalla Shaib Kaim leo Julai 14, 2023 amezindua barabara ya Lami Nzito na Zege Magomeni- Kirumba- Kabuhoro- Ziwani wilayani Ilemela yenye urefu wa KM 0.9 iliyojengwa na Mkandarasi Nyanza Road Works.

Akizindua mradi huo ndugu Kaim ameupongeza Uongozi wa Manispaa ya Ilemelaa kwa usimamizi madhubuti wa kazi iliyogharimu zaidi ya Milioni 998 hali iliyopelekea ubora unaotakiwa na viwango thabiti vilivyotarajiwa.

"Mradi upo vizuri na umezingatia viwango" amesisitiza kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi baada ya kukagua barabara na kuridhika na ubora na viwango kutokana na thamani ya fedha iliyotumika.


Naye  Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Angelina Mabula amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Fedha za Mradi huo kwani barabara hiyo imeondoka kero kubwa ya usafiri kwa wananchi wa kata ya Kirumba hasa wa kwenye makazi ya miinuko.

Katika wakati mwingine, Kiongozi wa mbio za Mwenge amewapongeza Ilemela kwa kutekeleza vema Ujenzi wa wodi ya wajawazito kwa zaidi ya Milioni 199 kwenye Kituo cha Afya Buzuruga ambapo shughuli ya Uzinduzi wa jengo hilo ilienda sambamba na ugawaji wa vyandarua kwa akinamama katika hatua za kuwakinga dhidi ya ugonjwa wa Malaria.


Kabla ya kufika kwenye Mradi wa kugawa vifaa vya kufanyia usafi na zoezi la usafi kiloleli, Mwenge wa uhuru ulifika kwenye Shule ya wasichana ya Bwiru ambapo viongozi hao na wa wilaya walipanda miti ya matunda 3000 katika kuhamasisha uhifadhi wa mazingira na lishe bora na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru akahimiza utunzwaji.

Vilevile, Mwenge wa uhuru ulimulika mradi wa Vijana wa ufugaji kuku Nyasaka na ukapongeza Halmashauri kwa kuwapatia mkopo wa Milioni 15 kikundi hicho pamoja na kitoa elimu ya Ufugaji na wakatoa wito kwa Halmashauri kuwakopesha zaidi wakimaliza marejesho na mwisho ukaweka Jiwe la msingi kwenye Ujenzi wa Bweni la wanafunzi Buswelu shule ya msingi.

Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 inasema "Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Uchumi wa Taifa."

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.