• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BONANZA LA MICHEZO LA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA LAIMARISHA AFYA, MSHIKAMANO NA UTENDAJI KAZI

Posted on: December 20th, 2025

Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa kujenga utumishi wa umma ulio imara, wenye motisha, unaozingatia maadili na unaoleta tija kwa wananchi kupitia programu mbalimbali ikiwemo michezo kwa watumishi wa umma.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda wakati akifungua Bonanza la Michezo kwa watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka lililofanyika katika Viwanja vya CCM Kirumba, Jijini Mwanza, tarehe 20 Desemba, 2025.

Mhe. Mtanda amesema bonanza hilo ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya Serikali inayolenga kuhakikisha watumishi wa umma wanakuwa na afya njema ya mwili na akili, mshikamano kazini na uadilifu wa hali ya juu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Ameeleza kuwa majukumu ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka yanahitaji umakini mkubwa, uzingatiaji wa sheria, ujasiri wa kufanya maamuzi magumu na msimamo thabiti wa kimaadili. Hivyo, mazingira ya kazi yenye mshikamano na ushirikiano huchangia kwa kiasi kikubwa ufanisi wa taasisi.

Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa michezo na burudani ni nyenzo muhimu ya kuondoa msongo wa mawazo, kuimarisha afya na kujenga moyo wa kufanya kazi kama timu moja.

Aidha, amesema Serikali inatarajia matukio kama haya yaendelee kutumika kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi kati ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wadau wa haki jinai, jambo litakalosaidia mapambano dhidi ya uhalifu na rushwa.

Kwa niaba ya Serikali ya Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda ametoa wito kwa watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uzalendo kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.

Naye Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylivester Mwakitalu amesema bonanza hilo limeandaliwa kwa lengo la kuimarisha afya za watumishi pamoja na kuongeza ufanisi na ari katika utendaji kazi wa kila siku.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • NAIBU WAZIRI CHAYA AITAKA TISEZA KUSIMAMIA UAJIRI WA WATAALAMU KWA WAWEKEZAJI

    January 06, 2026
  • SERIKALI KUPANUA MASOKO YA DHAHABU KIMATAIFA

    January 05, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.