• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

COPRA YAKABIDHI MBEGU YA KISASA YA CHOROKO TANI 1.5 MWANZA

Posted on: October 24th, 2025

Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imekabidhi Mbegu ya kisasa ya Choroko tani moja na nusu kwa Wakulima wa Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kuzitumia katika msimu wa kilimo wa 2025 ambapo zitasaidia kuongeza uzalishaji.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano hayo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo tarehe 24 Oktoba, 2025 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Chagu Ngh’oma ameishukuru taasisi hiyo na akatoa wito kwao kuwatafutia masoko wakulima ili walime kwa manufaa.


Bwana Ngh’oma amesema choroko kwa kipindi kirefu limekua ni zao la chakula na kidogo biashara hususani katika wilaya za Kwimba na Misungwi ila ujio wa taasisi hiyo na mikakati yake unatarajiwa kuleta manufaa kwa wakulima kuzalisha zaidi na kuuza na hatimaye kukuza hata uchumi wao.

Ameongeza kuwa kwa msimu wa 2024/25 mkoa wa Mwanza ulipanga kupata tani elfu 30 za choroko ila ulipata tani elfu 27 sawa na 73% kutokana na changamoto kadhaa ikiwemo ya mbegu duni ila ujio wa mbegu hiyo ya kisasa utasaidia kufikia malengo kwani wakulima watakua na uhakika wa uzalishaji.


Aidha, amewataka wataalamu kuanzia ngazi za chini (maafisa Ugani) kusimamia ipasavyo ili kufikia malengo yaliyopangwa na kwamba itasaidia pia kuongeza mapato ya halmashauri kutoka kwenye zao hilo huku akibainisha kuwa kwa mwaka 2024/25 Kwimba ilikusanya milioni 300 na Misungwi ikijikusanyia Milioni 70.


Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Maendeleo ya Mazao ja Viwango COPRA Bi. Pendo Bigambo amesema taasisi hiyo imetoa mbegu hizo ili kuchagiza uzalishaji na amewataka wasimamizi kuzigawa mbegu hizo kwa kufuata muongozo wa mfumo ili kuwa na usawa.

Ameongeza kuwa kwa kanda ya ziwa taasisi hiyo kinara wa usimamizi mifumo ya uzalishaji na usimamizi wa mazao kwa mwaka huu imetoa tani 192 ya mbegu bora za zao hilo ili kusimamia uzalishaji, uchakataji na kwamba itahakikisha mkulima anapata soko la uhakika wa mazao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.