• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DKT. BITEKO ATOA WITO KWA WAHITIMU CHUO CHA SAUT KUWA WAZALENDO

Posted on: December 16th, 2023

DKT. BITEKO ATOA WITO KWA WAHITIMU CHUO CHA SAUT KUWA WAZALENDO


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe, Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Tanzania kwenda Kusaidia jamii kwa kutumia taaluma zao na kujiepusha na Rushwa ili kusaidia watanzania wasiojiweza na kuwainua kutoka kutoka sehemu walipo.

Dkt. Biteko ametoa wito huo leo tarehe 16 Disemba, 2023 wakati wa Mahafali ya Ishirini na Sita ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino cha Tanzania yaliyofanyika kwenye Uwanja vya Raila Odinga chuoni hapo ambapo kwa nafasi ya Ugeni Rasmi wanafunzi 3066 wamehitimu katika ngazi mbalimbali.

Mhe. Biteko amesema anatamani kuona taaluma zao wanazitumia kwa manufaa ya  kusaidia wenye uhitaji kwenye jamii kwa kutoa ujuzi na ubunifu kwa upendo na kwamba ili kutimiza hilo ni lazima wawe na hofu ya Mungu na wenye kutenda zaidi na sio kulalamika na kujihusisha na matendo ya Rushwa.


"Kusoma kwenu hakutathibitishwa kwa cheti mlicho nacho Mkononi bali kwa athari ya matendo yenu baada ya kuhitimu kule muendako, namna ya kukabiliana na matatizo au jinsi ya kusaidia jamii kupitia taaluma zenu na kwakua kule muendako kuna mapambano basi wenye nguvu watasimama na walio dhaifu wataachwa njiani." Dkt. Biteko.


Akijibu hotuba ya Makamu Mkuu wa chuo hicho, Mhe. Biteko ameahidi kuwa Serikali itarekebisha Barabara za Mitaa ambazo zina makorongo na amebainisha kuwa siku za usoni chuoni hapo zitawekwa taa kwa ajili ya kuweka mazingira salama ya wanafunzi hasa usiku na kwamba Mkandarasi wa Ujenzi huo ameshapatikana.

Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Cha SAUT, Askofu wa Jimbo Katoriki la Geita na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoriki Tanzania, Askofu Flavian Kasala amesema Baraza la Chuo hicho linamshukuru Rais Samia kwa Ulezi wa Vyuo nchini kupitia TCU na Bodi ya Mikopo na anaamini kuwa Viwango vya Udahili na Mikopo kwa wanafunzi itaongezeka ili kuendelea kuboresha Elimu Nchini.


Aidha, ametumia wasaa huo kuwasihi wahitimu kuenenda kimaadili huko waendako kwa mujibu wa walivyolelewa na kwenda kukitangaza Chuo hicho kwa kuwa weledi na wenye ujuzi na ubunifu mkubwa katika kazi na kwamba kwa ambao hawataajiriwa waende wakatunie ujuzi walioupata kufanya kwa vitendo kile walichojifunza.

Balozi Prof. Costa Ricky Mahalu, Makamu Mkuu wa Chuo hicho amebainisha kuwa kwenye Mahafali hayo wamehitimu jumla ya wanafunzi 3066 katika fani mbalimbali katika ngazi za Astashahada hadi Shahada ya Udaktari wa Falsafa ambapo 49% ni wanawake na 51% Wanaume na kwamba Maadili na Taaluma ndio nguzo ya Chuo hicho kwenye kutoa Elimu bora.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.