• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Filamu ya ROYAL TOUR kutangaza Vivutio vya Utalii Mwanza

Posted on: June 11th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel amewakaribisha wananchi wa Mkoa huo kwenye kuitambulisha rasmi kwa kuiangalia filamu ya Royal Tour hafla itakayofanyika kwenye Viwanja vya Rock Ciy siku ya tarehe 18 Juni 2022.


Akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari mapema leo, Mkuu wa Mkoa amesema  Utambulisho huo rasmi utatanguliwa na shughuli mbalimbali ambapo Juni 16, 2022 watu zaidi ya mia moja watatembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na tarehe 17,06, 2022 kutakua na ziara ya kutembelea vivutio vya utalii vya Jiji la Mwanza na Safari za Ziwani.


"Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imeandaa tukio hili mahsusi kwa ajili ya kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hasaan kuitambulisha Sekta ya Utalii nchini ya kuvitangaza Vivutio vya Utalii na utamaduni wetu" amefafanua Mkuu wa Mkoa.


Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amebainisha kuwa Filamu ya Royal Tour mpaka sasa imetazamwa na watu wa Mataifa mbalimbali Duniani hivyo kutakua na ongezeko la idadi ya Watalii wanaotembelea nchi yetu na kuongeza pato la nchi sambamba na uwekezaji kwenye sekta mbalimbali.


"Kupitia kuitambulisha rasmi filamu ya Royal Tour Mkoani Mwanza watapata fursa ya kutembelea vivutio vya Utalii kama Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saa nane, Jiwe la Bismark, Gunzert House na malumbusho ya Kabila la wasukuma ya Bujora."


Mhe Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa Filamu ya Royal Tour iliyofanywa na Mhe Rais Samia Suluhu Hasaan imeonesha vivutio vya utalii nchini kama vile Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Ngorongoro, Fukwe za Zanzibar, utalii wa utamaduni pamoja na Madini ya Tanzanite.


"Utambulisho rasmi wa Filamu ya Royal Tour Mkoani Mwanza utautambulisha Mkoa kama lango kuu la kuingilia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ukizingatia kwamba inawachukua Watalii takribani saa mbili na nusu kufika kwenye Hifadhi hiyo wakitokea Mwanza," amesema.


Vilevile, Mkuu wa Mkoa amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi za kuboresha Miradi mikubwa itakayokuza na kuendeleza Utalii Mkoani Mwanza kupitia Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Mwendo Kasi, Ujenzi wa Daraja la Busisi na ukarabati mkubwa wa Uwanja wa ndege wa Mwanza hususani kwenye ujenzi wa jengo la abiria.


Utambilisho wa Filamu hiyo yenye dakika 56 Mkoani Mwanza utatanguliwa na burudani kutoka vikundi vya ngoma za asili na wasanii mbalimbali kuanzia saa 9 Alasiri hadi saa 1 jioni na utakuwa na washiriki takribani 1000.


_Mwisho_

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.