• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Halmashauri zilizopo Kanda ya ziwa zatakiwa kuhakikisha kamati za Fedha zinajengewa Uwezo

Posted on: September 19th, 2023

Halmashauri zilizopo Kanda ya ziwa zatakiwa kuhakikisha kamati za Fedha zinajengewa Uwezo


Halmashauri za Mikoa ya Kanda ya ziwa zimetakiwa kuhakikisha Kamati za Fedha, Uongozi na Mipango zinapatiwa mafunzo ili kuwajengea uwezo Waheshimiwa Madiwani wa kamati hizo kuzisimamia Halmashauri zao kwa ufanisi.

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 19 Septemba 2023 na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Miundombinu, Mbunifu Majengo Chagu Nghoma kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza wakati akifungua mafunzo ya Kamati hizo yaliyoandaliwa na Chuo cha Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na Ofisi ya Raisi TAMISEMI.

Amesema, ili ipatikane tija kwenye utekelezaji wa majukumu ya kamati hizo Mhe. Makamu wa Rais kupitia Mkutano wa 37 wa ALAT uliofanyika Mwezi Mei mwaka huu aliagiza kupatiwa mafunzo elekezi kwa kamati hizo lakini kumekua na uzembeaji wa kushiriki mafunzo yanayoandaliwa na Chuo cha Serikali za Mitaa jambo ambalo halikubaliki.

Chagu amefafanua kuwa, ili waheshimiwa Madiwani waweze kuzisimamia vema Halmashauri zao hususani taratibu, kanuni na sheria za usimamizi wa fedha ni lazima wajumbe wa Kamati hizo wajengewe uwezo mara kwa mara wa juu ya msingi wa kisheria wa uwepo wa kamati hizo na majukumu yake hivyo, Halmashauri hazipaswi kubaki nyuma kwenye hilo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa (Hombolo), Mkuu wa Kampasi ya Shinyanga (SHYCA) Dkt. John Kasubi amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuzijengea uwezo kamati hizo ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu kwenye Halmashauri zao.

Aidha, amefafanua kuwa mafunzo hayo yanayoendelea kwa wakati mmoja kwenye Mikoa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Kati na Ziwa ni muendelezo wa utekelezaji wa agizo la Mhe. Makamu wa Rais kwani tayari yalishatolewa kwenye Kanda ya Kaskazini na Mashariki na kwamba Chuo cha Serikali za Mitaa ndio Chuo kiongozi katika kuzijengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mitaa na ndio wafundishaji wa mafunzo hayo.

Vilevile, Dkt. Kasubi ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi kuwapeleka vijana wao kujiunga na chuo hicho katika kampasi zake zilizopo Hombolo, Dodoma mjini na Shinyanga kilichopo Kanda ya Ziwa mkoani Shinyanga ili waweze kupata elimu katika ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada katika fani mbalimbali.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.