• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HISTORIA YAANDIKWA DARAJA LA J.P MAGUFULI LAFUNGULIWA RASMI

Posted on: June 19th, 2025

HISTORIA YAANDIKWA DARAJA LA J.P MAGUFULI LAFUNGULIWA RASMI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo juni 19, 2025 amezindua na kufungua rasmi daraja la J.P Magufuli lenye urefu wa Kilomita tatu lililojengwa na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporationi (CCECC) kwa gharama ya Shilingi bilioni 718 pamoja na VAT.

Akizungumza na wananchi katika hafla ya ufunguzi iliyofanyika katika viwanja vya chuo cha ufundi Kalwande wilayani Misungwi Mhe. Rais amesema serikali imejidhatiti katika kuwaletea wananchi uhakika wa usafiri na usafirishaji na ndio maana kwa nyakati tofauti imeendelea kuboresha vivuko na hatimaye ujenzi wa daraja.

Dkt. Samia amesema, tangu aingie madarakani amehakikisha anakamilisha ndoto za hayati Rais wa awamubya tano ikiwemo kukamilisha miradi ya kimkakati ukiwemo daraja hilo na kwamba anayo furaha kufuta historia zenye huzuni za usafiri duni za wananchi kutumia muda mrefu kuvuka upande mmoja hadi mwingine na kwa sasa watu watatumia dakika 4 tu.

Aidha ametoa wito kwa jamii, wizara ya Ujenzi pamoja na vyombo vya ulinzi kulilinda daraja hilo na akawasihi wananchi kuongeza uzalishaji kwenye kilimo, ufugaji na biashara ili kuongeza tija kwenye maisha yao kwani daraja litaleta fursa ya kuimarisha biashara ya kikanda baina ya Tanzania na nchi za jirani.


Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amemshukuru Mhe. Rais kwa kuandika historia ya upendo kwa kuendeleza ujenzi wa daraja la JP Magufuli kutoka asilimia 25 hadi 100 ikiwa ni kwa kulipa zaidi ya bilioni 450 akiwa amekuta yamefanyika malipo ya bilioni 250 tu.

Amesema kuwa daraja hilo ni alama kwa taifa na kwamba kanda ya ziwa inakwenda kuchechemka kiuchumi kwa makundi yote ya wafanya biashara na wajasiriamali kwani linafunganishwa na huduma zingine za uchukuzi kutoka mradi wa SGR kupitia kituo cha Fella kilichopo Kilomita 15 tu kutoka darajani.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru na Mhe. Rais kwa kuipatia Mwanza zaidi ya Trilioni 5.6 za miradi ya maendeleo (minne 4) na akabainisha kuwa daraja hilo litaongeza mchango wa Mkoa wa Mwanza kwenye pato la Taifa ambapo kwa sasa unachangia zaidi ya Trilioni 7 ambazo ni asilimia 7.2.

Aidha, amefafanua kuwa vivuko vilivyokua vikitumika kuvusha vitahamishiwa sehemu zingine kwa ajili ya kuimarisha huduma mathalani MV Misungwi kitapelekwa Kisorya na Rugezi na MV Sengerema kitawavusha wananchi wa visiwa vya Kanyala- Kasarazi wilayani Sengerema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA DARAJA LA J.P MAGUFULI LAFUNGULIWA RASMI

    June 19, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.