• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HUDUMA YA MAJI IMEANZA KUREJEA - RC MTANDA

Posted on: September 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema huduma za maji mkoani humo zimeanza kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya wataalamu kutoka Mamlaka ya Maji na Usafi na Usafi wa Mazingira (MWAUWASA) na Shirika la Ugavi (TANESCO) kurekebisha tatizo.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 25 Sptemba, 2025 kwenye Chanzo cha Maji cha Butimba wilayani Nyamagana alipofika kufanya ukaguzi kwenye mitambo ya kuzalisha na kusambaza maji ambayo ilipata hitilafu takribani siku nne zilizopita.

Mhe. Mtanda amesema mafundi wamefanya kazi mchana na usiku kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kama kawaida na wamefanikisha hilo kwa kurejesha mawasiliano ya umeme kwenye pampu ya kusambaza maji kutoka kwenye chanzo hicho kwenda kwenye matenki.

“Changamoto iliyojitokeza hapa ni umeme kutofika kwenye pampu yaani kilichokua kimekwama ni mawasiliano ya umeme kufika kwenye pampu lakini kwa juhudi na ushiriniano wa wataalamu wetu napenda niwaambie wananchi kwamba tayari kazi ya matengenezo imekwisha.” Mhe. Mtanda.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwashukuru wataalamu wa Mamlaka hiyo ya Maji pamoja na TANESCO kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mitambo inarejea katika hali ya kawaida na kwa kuweka mfumo ambao hautoruhusu mitambo ya maji kuathirika na hitilafu ya umeme endapo litatokea.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewashukuru wataalamu kutoka wizara hiyo kwa kushirikiana na MWAUWASA pamoja na TANESCO kwa kufikisha nishati ya umeme kwenye pampu kama awali.

“Mhe. Mkuu wa Mkoa, kwakweli mafundi na wataalamu wetu wamefanya kazi kubwa na niwakikishie tu wananchi kuwa tumewasha pampu na sasa wananchi tayari wameanza kupata huduma ya maji kama ilivyokua siku za nyuma.” Katibu Mkuu

Mbali ya hayo Mhe. Mkuu wa Mkoa akiwa ameambatana na Katibu Mkuu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA walihitimisha ziara kwa kuwatembelea Kiwanda cha Dawa, Zahanati na kwenye Makazi ya wananchi wa Buhongwa ambapo wamejiridhisha kwamba Maji yanatoka tena kwa kasi inayotakiwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.