• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KAMATI YA MTAKUWWA MWANZA YATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WA KULINDA JAMII DHIDI YA UKATILI

Posted on: August 13th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza ndugu Balandya Elikana amewataka wajumbe wa kamati ya ulinzi wa wanawake na watoto (MTAKUWWA) mkoani humo kushirikiana na serikali kuhakikisha wanatambua na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazokabili makundi hayo na kuwaondoa kwenye ukatili.


Ndugu Balandya amesema hayo leo Agosti 13, 2025 wakati akizindua mafunzo ya siku tatu kwa kamati ya Mkoa ya kupinga na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto NPA-VAWC 2024/25- 2028/29 II.


Amesema ni lazima mwanakamati azunguke kwenye jamii ili kubaini changamoto mbalimbali zinazowakwamisha katika kushiriki kwenye kujenga uchumi wao na kuhakikisha wanaweka misingi ya kuondoka changamoto hizo.

"Ukatili kwa wanawake na watoto unazuia maendeleo kwa jamii na nchi kwa ujumla kwani serikali inalazimika kuahughulika na majeraha ya ukatili kama kutibu na kunasihi, hivyo wajumbe nawaomba mkatekeleze wajibu wenu." Amesema Balandya.


Ameongeza kuwa mchanganyiko wa wajumbe kutoka kwenye taasisi na madhehebu ya dini mbalimbali umelenga kuyafikia makundi mbalimbali na kuhakikisha jamii yote inafikiwa na kupatiwa elimu dhidi ya ukatili.


Akizungumzia watoto wanaoishi mtaani, Katibu tawala amesema kila mmoja kwenye eneo lake ahakikishe anafikisha ujumbe kwamba ni vibaya kuwahudumia watoto wanaoomba pesa mtaani kwani inapelekea kuwafanya waendelee kuwepo.


Akimuwakilisha Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Gabriel Mashauri amebainisha kuwa kwa siku tatu wajumbe watapitishwa katika maeneo 8 ambazo ni afua za kufuata na mwisho wa mafunzo hayo kila mjumbe atajua majukumu yake ya kila siku katika kuhakikisha watoto na wanawake wanakingwa na ukatili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA MTAKUWWA MWANZA YATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WA KULINDA JAMII DHIDI YA UKATILI

    August 13, 2025
  • ZAIDI YA WALENGWA ELFU HAMSINI WANUFAIKA NA RUZUKU YA BILIONI 82 MWANZA

    August 13, 2025
  • WARATIBU WA TASAF WAAGIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA UKAMILIFU NA UTIMILIFU

    August 12, 2025
  • RC MTANDA AKITETA JAMBO NA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

    August 11, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.