• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KUFUATIA MTAALA MPYA RAS MWANZA ATOA MAAGIZO KWA WATENDAJI SEKTA YA ELIMU

Posted on: February 5th, 2025

KUFUATIA MTAALA MPYA RAS MWANZA ATOA MAAGIZO KWA WATENDAJI SEKTA YA ELIMU


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amewataka watendaji sekta ya elimu kuhakikisha wanabadilika na kujifunza namna ya kutekeleza mtaala mpya ulioboreshwa ili waweze kuelewa na kutekeleza mabadiliko hayo yaliyoanza kutumika Januari 2025 kwa ufanisi katika Shule zao.

Ametoa agizo hilo mapema leo Jumatano Februari 05, 2025 Wilayani Sengerema wakati akifungua kikao cha Maafisa Elimu na wadhibiti ubora walioketi kutathmini utekelezaji wa shughuli za Elimu kwa mwaka 2024 na kuweka malengo ya kufanya vizuri zaidi.

Aidha, RAS Balandya amewataka kutathmini ubora na udhaifu wao na kuweka mikakati bora ya kufanya vizuri zaidi na kwamba wasibweteke kwa kuwa Mwanza imefanya vizuri kitaaluma katika mitihani yote hususani wa kidato cha nne ambapo ufaulu ni wa 98.2%.

Ili kuendelea kuwa bora, Ndg. Balandya amewataka wataalamu hao kuweka mikakati ya namna ya kukabili changamoto zinazorudisha taaluma nyuma kama wanafunzi kumudu stadi za kusoma, kuhesabu na kuandika pamoja na ufundishaji duni ili kubaki juu kitaaluma.

Pia amewataka maafisa hao kuweka mpango wa kufanikisha Mkoa kufanya vizuri zaidi  kwenye michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA 2025 na kuendelea kusimamia fedha za ujenzi wa miundombinu bora ya elimu ambapo amebainisha kuwa mwaka 2024 Elimu Msingi imepokea zaidi ya Bilioni 24 na kwa sekondari Bilioni 17.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Mwalimu Martin Nkwabi amebainisha kuwa 2024 ulikua mwaka mzuri mathalani katika uboreshaji miundombinu, taaluma kwa mitihani ya upimaji na mitihani ya Taifa na hata katika michezo kwani Mwanza imeibuka kidedea.

Vilevile, amesema kiwango cha kuweka wanafunzi shuleni kimepanda kutoka 7% mwaka 2023 hadi 4% mwaka 2024 hivyo kiwango cha kuwafanya wanafunzi wadumu darasani ni kikubwa na kimefuta mdondoko.

Ujio wa mtaala mpya ulioboreshwa ni katika kutekeleza agizo la Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuboresha mitaala ya Elimu Msingi, Sekondari na Ualimu ili kuwawezesha wahitimu kuwa na ujuzi wa kujiajiri na kuajiriwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.