• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kwimba Yahitaji Msukumo wa Maendeleo

Posted on: August 16th, 2018

MKuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Senyi Ngaga kuendeleza kazi zilizokuwa zinafanywa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Mtemi Msafiri ikiwemo kukomesha  mauaji ya kishirikina, kupambana na wauzaji na watengenezaji wa  pombe  haramu (gongo) na kuzuia uharibifu wa kukata miti na kuchoma mkaa bila kufuata taratibu.

Mhe.Mongella ameyasema hayo leo Agosti 16 mara baada ya kumuapisha Mkuu wa Wilaya ya kwimba Mhe.Senyi Simon Ngaga katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

"Uende kuitafsiri nafasi uliyopewa na Mhe. Rais Dkt.John Magufuli kaendeleze vita dhidi ya mauaji ya kishirikina japo yamepungua ikiwezekana yaishe kabisa," alisema Mongella.

Mhe.Mongella aliongeza kuwa Kwimba ndiyo wilaya ya mwisho kimaendeleo Mkoani Mwanza kati ya Wilaya saba hivyo anahitaji aone mabadiliko ya kimaendeleo katika Wilaya ya hoyo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo   Mhe.Ngaga ameomba  ushirikiano kutoka kwa watumishi na wana mwanza kwa ujumla ili afanikishe malengo  ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Hata hivyo alikabidhiwa vitendea kazi ambavyo ni  Katiba ya Jamuhuri ya vya Muungano wa Tanzania 1977,ilani ya uchaguzi wa Mwaka 2005,Sheria za Mitaa ya Mwaka 1977 pamoja na Masharti ya Mkuu wa wilaya ya Mwaka2016.

Awali Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Sam Rumanyika amesema anahitaji ushirikiano katika mahama kwa wananchi na watumiahi wote kwani wanaapa kuwa waadilifu.

 "Viapo vikifuatwa mnakuwa watumishi wazuri,kwani ni uadilifu mkubwa, tumekusudia kuondoa kesi za muda mrefu na pia tumezindua kampeni katika Mkoa wa Geita,Mara na Mwanza ambao una misingi mnne itakayotusaidia katika Mahakama na wateja wetu,"alisema Mhe.Rumanyika.

"Haki yako Wajibu wangu, Napenda kesi nachukia Mrundikano, Kila mtu atende wajibu wake na Mrundikano wa Kesi ni Sumu ya Nchi"alisema Mhe. Rumanyika.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Mnec )wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Jamal  Abdul Babu alisema kila mtu anastahili kutii Mamlaka iliyopo madarakani na utelekezaji wa ilani utasaidia watu wachape kazi.

Aidha Mhe.Mongella alisisitiza  ukusanyaji wa mapato,utumiaji mzuri wa ardhi,kuwe na siasa safi, uongozi bora na kuwe na mkakati wa kuondoa umasikini hivyo italeta mshikamano na Maendeleo katika  Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.