• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

Posted on: September 11th, 2025

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewataka wataalamu wa taaluma ya Ufuatiliaji na Tathmini kuimarisha zaidi mifumo ya kiutendaji ili kuwa kada imara.

Ametoa maagizo hayo mapema leo tarehe 11  Septemba, 2025 wakati akizindua kongamano la nne la Ufuatiliaji, tathmini na kujifunza lililowakutanisha wataalamu zaidi ya 1200 kutoka ndani na nje ya nchi kwa zaidi ya mataifa 18.

Amesema ni lazima wataalamu hao wajikite katika ubunifu na kujiendeleza kitaaluma ili wapate stadi za kisasa za kusimamia miradi na kujisahihisha ili kuwa na uwajibikaji bora katika kusimamia miradi ya maendeleo.

"Kukamilika kwa mradi mkubwa wa Daraja wa JP Magufuli lenye urefu wa Kilomita 3, Meli ya MV Mwanza, Stendi za Mabasi Nyamhongolo na Nyegezi, Chanzo cha Maji Butimba, Soko la mjini kati na kipande cha Isaka -Mwanza (SGR) ni matunda ya ufuatiliaji na tathmini uliofanyika kwa kina." Mhe. Majaliwa.

Dkt. Jim Yonazi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) amesema serikali imeanzisha idara maalumu ya kufanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya serikali nchini ndani ya wizara, Sekretarieti za Mikoa na Halmshauri kama hatua za kuboresha mfumo wa sekta hiyo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameueleza umma huo kuwa Mkoa wa Mwanza unachangia pato la taifa kwa asilimia 7.2 na kushika nafasi ya pili kitaifa na kwamba ni kitovu cha biashara kwa nchi za maziwa makuu na kwamba mkutano huo utaacha athari chanya kibiashara na kukuza uchumi.

"Ndani ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan fedha takribani Tshs. Trilioni 5.6 zimeelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati na maendeleo na uwanja wa ndege wa Mwanza upo kwenye maboresho makubwa ya kuufanya kuwa wa Kimataifa." Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI YA BILIONI 1.3 KWA JESHI LA POLISI

    September 12, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI NCHINI

    September 11, 2025
  • MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

    September 11, 2025
  • NSSF WAFANYA ZIARA YA UWEKEZAJI MWANZA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.