• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Makamu wa Rais Dkt Mpango aiagiza MWAUWASA kuongeza uzalishaji chanzo cha maji Butimba-Mwanza

Posted on: September 14th, 2022


Leo Septemba 14, 2022, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ameweka Jiwe la Msingi kwenye Mradi wa Ujenzi wa Chanzo na Kituo cha Tiba ya Maji cha Butimba Mkoani Mwanza utakaogharimu Shilingi Bilioni 69.

Akizungumza na wananchi Dkt. Mpango ameiagiza MWAUWASA kupitia Wizara ya Maji kuongeza uzalishaji wa Maji kutoka kwenye chanzo hicho na kutoishia kwenye kuzalisha lita Milioni 48 pekee kwa siku ili kupata Maji mengi zaidi na kuweza kuondoa kero ya maji kwa wananchi walio wengi hasa wanaoishi kwenye maeneo ya miinuko.

Vilevile, amewaagiza Wizara ya Maji kuhakikisha wanaunganisha huduma ya Maji ndani ya siku saba tangia kuwasilishwa kwa maombi na kuacha tabia ya kubambikiza ankara za maji zenye gharama kubwa kwa wateja tofauti na uhalisia ili kuiondolea mamlaka hiyo malalamiko kutoka kwa wananchi.

Vilevile, Makamu wa Rais amewaagiza watendaji kwenye Halmashauri kuongeza nguvu kwenye Ukusanyaji wa Mapato ya ndani na kusimamia miradi kwa umakini na Uzalendo ili iweze kuendana na thamani ya fedha zinazotumika na kuweza kuwaondolea adha wananchi.

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso amemshukuru Makamu Rais kwa kuwajali wananchi wa Mwanza na kuelekeza uharakishaji wa Mradi huo na amebainisha kuwa kutokana na kikao kilichoketi baina na Wizara na Mkandarasi, Mradi huo utakamilika ifikapo Disemba 2022 badala ya mwezi februari 2023 iliyosainiwa hapo awali.

Naye, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMl) Mhe. Innocent Bashungwa amesema ahadi ya kumtua Mama Ndoo Kichwani ni lazima iende sambamba na kampeni ya Usafi wa Mazingira hivyo wananchi waongeze kasi ya kufanya Usafi kwenye mazingira yao ili kuweka miji katika Mazingira safi na kuweza kutunza Afya zao.

Waziri wa Mazingira, Mhe. Dkt. Seleman Jafo ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanatunza Mazingira kwa kupanda Miti na kuacha kutumia Mifuko ya Plastiki kwani mifuko hiyo inachafua vyanzo vya maji na inaharibu mitambo, hivyo wizara yake inandelea na kampeni ya kukamata mifuko hiyo ambayo hadi sasa imekamata tani 43.8.

Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga amesema kuwa mradi huo unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) ni sehemu ya utekelezaji wa Miradi mikubwa kwenye ukanda wa ziwa Viktoria na ulianza kutekelezwa Januari Mosi 2021 na utakamilika Mwezi Februari 2023 chini ya Mkandarasi Kampuni ya M/S Sogea Satom kutoka Ufaransa kwa Bilioni 69.

Mhandisi Sanga amebainisha kuwa Wizara imewaelekeza MWAUWASA kuongeza nguvu ya usimamizi na Mkandarasi kuongeza Rasilimaliwatu kwenye mradi huo ambao kwa awamu ya kwanza unatarajiwa kuzalisha lita milioni 48 kwa siku ili ukamilike kabla ya muda na kuweza kuboresha huduma ya upatikanaji wa Maji Safi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amesema Mradi huo unatarajia kuwa suluhu ya Mgao wa Maji hasa kwa wananchi waishio kwenye miinuko kwani utaongeza lita Milioni 140 kwani hadi mwisho wa mwaka 2021 kulikua na upungufu wa Lita milioni 70 kutokana na MWAUWASA kuzalisha Lita Milioni 90 pekee wakati mahitaji ni Lita Milioni 160.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.