• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mhe. Mongella aweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Kamanga

Posted on: January 19th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella ameweka jiwe la msingi Kituo cha Afya cha Kamanga  kilichojengwa kwa ushirikiano  baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Shirika lisilo la Serikali  lijulikanalo kama  CEDAR FOUNDATION  lenye Makao Makuu yake Nchini Uswisi kwa Tanzania lina Ofisi  yake Jijini Mwanza.

Ujenzi wa Kituo hicho ulianza Februari 2015 na kumalizika Novemba 2017 ambapo ujenzi huu unafanyika kwa awamu, na kwa sasa limejengwa jingo la wagonjwa wan je lenye vyumba 23 na nyumba 9 za watumishi,hadi kukamilisha Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ilichangia Jumla ya Shilingi 59,126,098.50 ambapo kati ya hizo  52,693,000 zilitumika kutengeneza mfumo wa maji na Shilingi 3,800,000 ziliweka mfumo wa umeme  wakati  1,433,097.50 zilitumika kulipia hati miliki ya eneo na Shilingi 1,200,000 zilitumika kupima eneo la kituo.

Shirika la CEDAR FOUNDATION limechangia jumla ya Shilingi bilioni 2.325 ambapo   fidia kwa waliokuwa wakazi wa eneo hilo ni shilingi milioni 251, ujenzi ni shilingi bilioni 1.55, tofauti na ujenzi Shirika limetoa vifaa tiba vyenye thamani ya ya Shilingi milioni 331 ikiwa ni gharama ya vifaa hivyo na usafirishaji,pia imegharamia vifaa vya ofisi kama jenereta,mashine ya kuchomea taka hatarishi na kufunga mfumo wa kielektroniki kwa thamani ya shilingi milioni 193.

Mhe.Mongella awali akiwapongeza wafadhili hao amesema kuwa, Mradi huu unategemea kutoa huduma bora za afya na ustawi wa wananchi zaidi ya watu elfu 30 wa kata ya Nyamatongo na kata nyingine za jirani, hivyo utasaidia vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.

 Mhe. Mongella ameongeza kuwa, pamoja na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali pamoja na wadau wa maendeleo Ikiwemo CEDER FOUNDATION, Sekta ya Afya Mkoa wa Mwanza inakabiliwa na changamoto mbalimabli ikiwa ni pamoja na upungufu wa watumishi wa afya kwa asilimia 51,ukowefu wa vituo vya huduma katika vijiji 303 na uwepo wa majengo ambayo hayajakamilika 109 katika vijiji na baadhi ya ya vituo vya huduma, upungufu wa nyumba za watumishi wa afya 951,ukosefu wa mashine muhimu za uchunguzi katika Mkoa(MRI), mwitikio mdogo wa jamii kujiunga na mfuko wa afya ya jamii CHF ambapo kwa sasa ni 10.89% ya waliojiunga  na o.71%(TIKA) lengo likiwa ni asilimia 30.

Hata hivyo, katika kukabiliana na changamoto hizi Mkoa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo unaendelea kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za afya, ununuzi wa vifaa muhimu vya uchunguzi wa magonjwa, ufungaji wa mifumo ya kielektroniki katika vituo vyote vyenye umeme na kutenga nafasi za ajira kila mwaka.

Aidha, Mkoa umepokea Bilioni 2.62 kwa ajili ya upanuzi wa vituo vya afya Mkoani Mwanza hivyo utahusisha ujenzi wa majengo ya huduma za upasuaji wa dharura za uzazi, wodi za wazazi, maabara na nyumba za watumishi utakaotekelezwa katika vituo 6 vya afya, ambapo ujenzi wa awamu ya kwanza umeanza katika vituo viwili vya Kahangara –Magu  na Karume – Ilemela na awamu ya pili itahusisha vituo vya Afya vya Bwisya – Ukerewe na Malya – Kwimba, Kome- Buchosa na Kagunga – Sengerema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.