• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MIUNDOMBINU BORA YA SHULE YAONGEZA HAMASA YA UANDIKISHAJI WANAFUNZI NYAMAGANA

Posted on: January 9th, 2024

MIUNDOMBINU BORA YA SHULE YAONGEZA HAMASA YA UANDIKISHAJI WANAFUNZI NYAMAGANA


*Uandikishaji wa wanafunzi wavuka matarajio shule za awali na msingi*


*RC Makalla amshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa madarasa*


*Shule mpya ya Kanenwa yawapunguzia watoto adha kutembea umbali mrefu*


*RC Makalla aagiza umeme na maji kupelekwa kwenye shule mpya*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amekagua miundombinu ya elimu ya awali, msingi na sekondari wilayani Nyamagana pamoja hali ya uandikishaji wa wanafunzi ambapo amebaini kuwa ujenzi wa miundombinu bora umepelekea uandikishaji wa wanafunzi kuvuka lengo la matarajio

Akiongea katika nyakati tofauti wilayani humo leo tarehe 09 Januari 2024, Mkuu wa Mkoa amesema matokeo ya usajili wa wanafunzi yanatokana na nia njema ya Serikali ya awamu ya sita ya kuhakikisha miundombinu kwenye shule za msingi na sekondari inaimarika ili kuwa na mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia.

Kutokana na ujenzi wa shule mpya ya msingi Kanenwa Mhe. Makalla amebainisha kuwa si tu imevunja rekodi ya uandikishaji kwa wanafunzi wa awali (Maoteo 150, walioandikishwa 350) na darasa la kwanza (Maoteo 200, waliosajiliwa 250) bali itaondoa adha ya watoto kutembea umbali mrefu kwenda kwenye shule za Bujingwa na Bukaza.

"Leo ni siku ya pili tangia shule zifunguliwe, kuanzia walimu, uongozi wa kata na wilaya, wazazi na walezi nisisitize tuweke msukumo, ushawishi na ufuatiliaji wa wanafunzi waweze kuripoti shuleni." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa akiwa kwenye shule ya sekondari Mirongo ambayo wameripoti watoto 71 kati ya 223.

Vilevile, Mhe. Makalla ameongeza kuwa shule zote mpya ndani ya Mkoa huo zimesajiliwa na hali hiyo itasaidia kuwa na wigo mpana wa watoto kupata shule za jirani na akatumia wakati huo kuwaagiza TANESCO na MWAUWASA kupeleka huduma kwenye shule mpya ili kutoa fursa kwa wanafunzi na walimu kuwa na mazingira mazuri ya ujifunzaji na kufundishia.

Wakati akitoa pongezi na shukrani kwa Rais Samia kwa kuhakikisha elimu inakua bora nchini, Makalla amewapongeza uongozi wa wilaya na Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa miundombinu hususani ya madarasa ya ghorofa na kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shuleni kwa wakati mara tu muhula mpya wa masomo ulipoanza mapema wiki hii.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mhe. Stansilaus Mabula ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais kwa kumwaga pesa nyingi kwenye uboreshaji wa miundombinu ya elimu na kuwapongeza watendaji wote ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa ushirikiano uliopelekea ukamilishaji bora wa miundombinu ya shule.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.