• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MIUNDOMBINU YA MICHEZO ISIWE YA KIBINAFSI- RC MTANDA

Posted on: December 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amezitaka taasisi zote zenye miundombinu rafiki ya michezo mkoani humo kuacha ubinafsi na kushirikiana na wadau wa michezo pale wanapohitaji kutumia miundombinu hiyo kwa maendeleo ya sekta hiyo.

RC Mtanda ametoa wito huo leo Desemba 21, 2025, alipokuwa akifunga Mashindano ya Rolling Stone Championship 2025, yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Nsumba Jijini Mwanza.

Amesema michezo kwa sasa ni sekta inayokua kwa kasi duniani, ikiwa na mchango mkubwa katika uchumi kwa kuzalisha ajira nyingi za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja, hivyo inahitaji kuungwa mkono kwa vitendo.

Akizungumzia mashindano hayo, RC Mtanda amesema Rolling Stone Championship 2025 ni jukwaa muhimu la maendeleo ya michezo nchini kwa kuwa yanalenga kuibua, kukuza na kulea vipaji vya vijana wenye umri wa miaka 9 hadi 21, sambamba na kuimarisha ushirikiano wa michezo kikanda.

Mhe. Mtanda ameahidi kuyasimamia mashindano hayo ili mwaka ujao yafanyike kwa mafanikio makubwa zaidi na kushirikisha kikamilifu nchi za Afrika Mashariki na Kati.

“Mwanza ni kitovu cha nchi za Maziwa Makuu, hivyo mashindano haya yana nafasi kubwa ya kuwa mashindano ya kweli ya Afrika Mashariki na Kati,” amesema.

Aidha, RC Mtanda amezitaka shule na taasisi zote zenye miundombinu ya michezo kuacha uchoyo na kuwakaribisha wadau wa michezo wanaohitaji kutumia maeneo hayo kwa shughuli za michezo.

“Niwapongeze uongozi wa Shule ya Nsumba kwa ushirikiano wao. Kama wasingewapkea na mngeweka makazi nje, gharama zingekuwa kubwa. Huu ni mfano wa kuigwa,” ameongeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa African Sports Park Centre, Bw. Hamis Alli, ambaye pia ni mratibu wa mashindano hayo, amesema Rolling Stone Championship ilianzishwa mwaka 2000 ikishirikisha nchi za Afrika Mashariki na Kati ikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Amesema kwa mwaka 2025, mashindano yameshirikisha Tanzania pekee, yakiwa na jumla ya timu 25 kutoka vituo 14 vya kulea na kukuza vipaji vya vijana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.