• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza wampongeza Mhe Rais Samia kwa kuboresha maslahi ya Wafanyakazi

Posted on: June 1st, 2022

Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ametoa rai kwa wafanyakazi wa taasisi na idara za serikali mkoani humo kufanya kazi kwa bidii, uzalendo na weledi ili kuuletea maendeleo Mkoa huo na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo leo kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa baada ya kupokea maandamano ya azimio la kumpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha maslahi ya watumishi kutoka kwa shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoani humo.

"Twendeni tukafanye kazi kwa uzalendo, itatuletea heshma kwa Mungu na kila mmoja akitekeleza majukumu yake tutakua tumemrudishia shukrani Mhe. Rais kwa vitendo na tusionekane kwenye wizi, ubadhirifu wala rushwa na haki ikainue maisha yetu."

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amewashukuru wafanyakazi hao kwa utashi wao kuthamini mema aliyoyafanya Mhe. Rais kwao kupitia utumishi wao na kwa pamoja wakaamua kutoa kauli ya kumpongeza kwa maandamano yenye furaha na bashasha.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi amesema Serikali ya awamu ya Sita  itaendelea kuwa sikivu hivyo ni wajibu wa kila mfanyakazi kufanya kazi kwa bidii katika eneo lake.


Akisoma risala ya Wafanyakazi Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoani Mwanza TUCTA,Zebedayo Athuman amesema shukurani ya Wafanyakazi kwa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ni kuchapakazi kwa bidii kwa lengo la kuliletea Maendeleo Taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi  Mkoani Mwanza,TUCTA  Yusuph Simbaulanga ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusikia kilio cha Wafanyakazi kitendo kitakachoongeza ari ya kazi.


Vilevile, Mhandisi Gabriel amewasihi viongozi wa wafanyakazi kushughulikia mara moja changamoto za wafanyakazi na kuwasilisha kwake zile zinazohitaji msaada zaidi wa ofisi yake na akaahidi kutoa ushirikiano.

"Kwa  mema yote haya yaliyofanyika tunalo deni kwa Mhe. Rais hivyo niwaombe viongozi wa shirikisho na viongozi wa vyama vya wafanyakazi isiwepo kero ya mfanyakazi yeyote bila kuifanyia kazi na kama kuna changamoto yoyote nitaifanyia kazi ili mfanyakazi yeyote akifika asubuhi kazini aanze kwa sala ya shukrani kwa mwenyezi mungu." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.