• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza waja na kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa Msingi na Sekondari

Posted on: July 22nd, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewataka Viongozi katika ngazi zote kuanzia kwenye Vitongoji kushirikiana kwa dhati kutekeleza Miradi ya Maendeleo kwenye maeneo yao shabaha ikiwa kuondoa changamoto zinazoikabili jamii.

Amesema hayo leo Julai 22, 2020 wakati wa Mkutano wa Wadau kuelekea Kampeni kubwa ya Ujenzi wa Miundombinu ya Vyumba vya Madarasa inayokwenda kuanza wiki ijayo Mkoani humo katika kuhakikisha wanafunzi kwenye shule za Msingi na Sekondari wanasoma kwenye madarasa bila kusongamana.

"Umoja ni nguvu, tunataka tuone kwenye majira haya ya mwanzo kabisa mwa mwaka wa fedha tunaazimia kwa pamoja kuwatoa watoto wa Shule za Msingi na Sekondari kwenye msongamano madarasani kwa kujenga vyumba vya madarasa vya kutosha." Amesisitiza.

Akifafanua suala la Elimu Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa huo kwa shule za Msingi una Mahitaji ya vyumba vya madarasa kwa zaidi ya elfu 18 na huku vilivyopo ni vyumba elfu 7 na kufanya kuwe na upungufu wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu 11 ikiw ni sawa na asilimia 59 huku Halmashauri ya Nyamagana ikiongoza kwa upungufu.

Vilevile, amebainisha kuwa kwa Shule za Sekondari Mkoa huo una upungufu wa zaidi ya vyumba vya Madarasa zaidi 750 na kwamba hali hiyo imemfanya kuitisha Mkutano huo Mkubwa wa Wadau kuhakikisha wanaweka Mkakati wa pamoja ili kumaliza tatizo hilo mara moja.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Ngusa Samike amebainisha kuwa Watendaji wote wako tayari kwa zoezi hilo nyeti na kwa hakika Mkoa unakwenda kulitekeleza kwa muamko mkubwa kwenye kila Halmashauri ili wanafunzi watakaoanza masomo mwakani watakupa mapinduzi makubwa sana kwenye suala la Miundombinu.

"Nikuhakikishie Mhe. Mkuu wa Mkoa kuwa Wabunge wote tumejipanga na tupo tayari kukuunga mkono kwenye kampeni hii, tutaenda kama timu na hakika Mwanza tunaanza safari hii leo na kwa hakika miezi sita baadae hatutakua sawa na sasa", amesema Mbunge Nyamagana, Mhe Stanslaus Mabula.

Mhe. Simon Mpandalume Diwani kutoka Magu ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) Mkoa amemshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kuja na Kampeni hiyo na amemhakikishia kuwa Waheshimiwa Madiwani wapo tayari kushirikiana naye kwa dhati katika kufanikisha adhma hiyo ya kizalendo.

Mkutano huo umehudhuriwa na  Waheshimiwa Wabunge, Taasisi za kifedha, Kamati ya Amani, Mabenki, Marafiki wa Mkoa, Wachimbaji wa Wauza Madini pamoja na Waziri wa Maji (MB) Mhe. Jumaa Aweso ambaye yupo kwenye ziara ya kukagua Miradi ya Maji Mkoani humo na amechangia Mifuko 200 ya Saruji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.