• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yanufaika na mradi wa utafiti wa kinga za malaria (PAMVERC) unaotekelezwa na Taasisi ya NIMR

Posted on: April 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel  amezindua Mrejesho wa Utafiti wa Vyandarua vyenye Viwatilifu vipya vya kuthibiti mbu wanaoeneza Malaria, wilayani Misungwi,  unaoonesha  maambukizi kushuka kutoka asilimia 51 mwaka 2018 hadi asilimia 21 sasa.

Hayo yamebainishwa Wilayani humo kupitia mradi wa utafiti wa kinga za malaria (PAMVERC) unaotekelezwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Kituo cha Mwanza, katika vijijini 72  na Kata 17 Wilayani humo.

"Nimearifiwa kuwa utafiti huu ulihusisha viwatilifu vipya aina ya Chloefenapyr ambavyo husababisha misuli ya mabawa ya mbu kukakamaa na hivyo kuzuia mbu asiruke au kutembea. Hii huzuia mbu asinyonye damu au kuruka kwenda kwa mtu mwingine, na hatimaye  kufa," amesema.

Sambamba na hilo, Mhe.Mhandisi Gabriel amewataka wananchi kuendeleza tabia ya usafi na utunzaji wa mazingira kuanzia sasa mradi huo unapoelekea ukingoni, ikiwemo kufyeka majani na kuziba madimbwi ili kuua mazalia ya mbu na hatimaye kudumisha jitihada za kuzuia malaria.

Mkurugenzi wa NIMR Kituo cha Mwanza

Dkt. Safari Kinung'hi amesema mradi huo wa miaka mitano (2018-2022) umetekelezwa Misungwi baada ya kiwango cha malaria kuonekana kuwa juu.

"Malaria kwa ujumla bado ni changamoto katika Kanda yetu hii ya ziwa. Tunaendelea na tafiti ambazo matokeo yake yatatumika kuondoa tatizo hili," amesema.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.